Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Mchengerwa Ampongeza Simbu Kutwaa Medali ya Fedha Jumuiya ya Madola
Jul 30, 2022
Na Jacquiline Mrisho

Na John Mapepele, Uingereza.

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa amempongeza mwanariadha Alphonse Felix Simbu kwa kushika nafasi ya pili na Hamis Mesai kushika nafasi ya nane kwenye mashindano ya mbio za Marathoni ya Jumuiya ya Madola yanayoendelea nchini Uingereza.

Mhe. Mchengerwa amesema kazi ushindi Simbu ni wa watanzania wote ambapo amewataka wanamichezo wote wanaoshiriki mashindano hayo kutanguliza uzalendo ili kuipeperusha bendera ya Tanzania kimataifa.

Kufuatia ushindi huo Simbu anajinyakulia zawadi ya dola za kimarekani 7500 kutoka Serikalini ikiwa ni ahadi aliyoitoa waziri Mchengerwa wakati akiiaga timu ya Tanzania.

Mara baada ya kushinda Simbu amesema anawashukuru watanzania kwa maombi yao ambayo yamemfanya ashinde katika mashindano hayo.

Amesema siri ya ushindi ni mazoezi ambapo amemshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan na Waziri Mchengerwa kwa kutoa msukumo wa pekee kwenye michezo.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi