Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

JMP Ashinda kwa Kishindo Uchaguzi Mkuu 2020.
Oct 30, 2020
Na Msemaji Mkuu


Zoezi la Utangazaji wa Matokeo ya Jumla ya Uchagzui wa Rais 2020, likiendeleo katika Kituo cha Mikutano kimataifa Julisu Nyerere(JNICC), Jijini Dar es Salaam ambapo Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (NEC), Mhe. Jaji Rufaa (Mst), Semistocles Kaijage, amemtangaza Dkt.John Pombe Magufuli wa CCM kuwa mshindi wa kiti hicho kwa kura zaidi ya 12,516,252 sawa na asilimia 84.4.

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC), Mhe. Jaji  Rufaa (Mst), Semistocles Kaijage akitangaza   matokeo ya jumla  Uchaguzi wa Rais ambapo Mgombea urais wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt.John Pombe Magufuli ameshinda kwa zaidi ya kura  milioni 12, kulia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi (NEC), Dkt.Wilson Mahera

Wakala wa moja kati ya vyama 15 ambavyo vimeshiriki Uchaguzi wa Rais 2020 akisoma fomu ya matokeo kabla ya kuijaza katika  zoezi la utangazaji wa matokeo ya jumla kwa Uchaguzi wa Rais 2020 kukamilika.

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC), Mhe. Jaji  Rufaa (Mst), Semistocles Kaijage akitangaza   matokeo ya jumla  Uchaguzi wa Rais ambapo Mgombea urais wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt.John Pombe Magufuli ameshinda kwa zaidi ya kura  milioni 12.

Mkurugenzi wa Uchaguzi (NEC), Dkt.Wilson Mahera akikabidhi fomu ya matokeo kwa mmoja kati ya mawakala wa vyama vilivyoshiriki Uchaguzi wa Rais 2020, ili aisome na kusaini kukubali matokeo ya Uchaguzi huo.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi