Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

CAG: Deni la Taifa ni Himilivu
Mar 29, 2018
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_29607" align="aligncenter" width="886"] Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG ) Prof. Mussa Assad akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu kauli yake aliyoitoa wakati akiwasilisha ripoti za Ukaguzi wa fedha kwa mwaka unaoishia June 30, 2017 kwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.Kulia ni Naibu mkaguzi mkuu wa hesabu za Taifa Bw. Athumani Mbuttuka na kushoto ni Naibu mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali anayeshughulia Mamlaka za Serikali za Mitaa Bw. Jasper Mero.[/caption] [caption id="attachment_29609" align="aligncenter" width="895"] Baadhi ya Waandishi wa Habari wakifuatilia mkutano wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG ) Prof. Mussa Assad uliofanyika leo mjini Dodoma.[/caption]

Frank Mvungi- MAELEZO, Dodoma.

Serikali imesema kuwa Deni la Taifa ni stahimilivu hali inayoonyesha kuendelea kuimarika kwa uchumi wa Taifa letu.

Akizungumza na waandishi wa habari leo mjini Dodoma  Mdhibiti na Mkaguzi  Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG ) Prof. Mussa Juma  Assad amesema kuwa hadi kufikia tarehe 30 June 2017 deni la taifa lilikuwa trilioni 46.08 ambapo deni  la ndani ni shilingi trilioni 13.34 sawa na asilimia 29.

Akifafanua amesema kuwa matokeo ya ukaguzi huo yatawekwa wazi mara baada ya ripoti husika kuwasilishwa  rasmi  Bungeni kabla ya tarehe 12, April  2018 na baada ya hapo nakala ngumu za vitabu zitapatikana kwenye Ofisi zote za Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali na kwenye tovuti (www.nao.go.tz).

 Kwa mujibu wa Ibara ya 143 (4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 (iliyorekebishwa mwaka 2005), mnamo machi 27, 2018 Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu  za Serikali (CAG), Prof. Mussa Juma Assad aliwasilisha ripoti ya ukaguzi wake kwa mwaka  wa fedha unaoishia  June 2017 kwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi