Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Bombardier Dash-8 Q400 Ilivyowasili Nchini
Apr 02, 2018
Na Msemaji Mkuu

Ndege ya tatu ya Bombadier Dash-8 Q-400  ikipigiwa saluti ya maji (Water Salute) mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere ikitokea Montreal, Canada na kupokelewa na umati mkubwa wa wananchi wakiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli leo Aprili 2, 2018

Ndege mpya ya Serikali aina ya Bombadier Dash-8 Q400 ikiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam leo Jumatatu April 2, 2018.

Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiwaongoza Viongozi wengine wa Serikali kukata utepe kuashiria uzinduzi wa ndege mpya ya Serikali aina ya Bombadier Dash-8 Q400 iliyowasili leo Jumatatu April 2, 2018 Jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipongezwa na Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Mashariki na Pwani Dkt.  Alex Malasusa baada ya kupokea ndege ya tatu ya Bombadier Dash-8  Q400  katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere ikitokea Montreal, Canada, leo Aprili 2, 2018 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akitelemka kutoka kwenye  ndege ya tatu ya Bombadier Dash-8 Q-400  ilipoipokea katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere ikitokea Montreal, Canada, leo Aprili 2, 2018 

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi