Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

AUWSA Yaleta Neema Itokanayo na Majitaka
Sep 13, 2022
Na Jacquiline Mrisho

Na Ahmed Sagaff, Arusha

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Arusha (AUWSA) inazalisha mkaa unaotokana na mabaki ya majitaka yanayosafishwa katika mabwawa yao.

Akizungumza leo jijini hapa, Mkurugenzi Mtendaji wa AUWSA, Mhandisi Justine Rujomba amesema mkaa huo unatokana na mradi wa kusafisha majitaka unaogharimu shilingi bilioni 15.

"Mkaa huo hauna harufu na unaweza kutumika kwa matumizi ya kawaida," ameeleza Mhandisi Rujomba.

Pamoja na hilo, amesema mabaki mengine ya majitaka ya kutoka viwandani yatatumika kutengeneza mbolea kwa ajili ya Kilimo cha nyasi za chakula cha mifugo.

Amesema mradi huo wenye mabwawa 18 yanatopokea majitaka kutoka viwandani, una uwezo wa kutibu lita milioni 22 kwa siku na kwamba mtandao wa majitaka una kilomita 268.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi