Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Oct 30, 2020
Na Msemaji Mkuu

Matukio katika Picha: Utangazaji Matokeo ya Uchaguzi wa Rais, JNICC Jijini Dar es Salaam.


Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC), Mhe. Jaji (Mst), Semistocles Kaijage akitangaza   matokeo ya Uchaguzi wa Rais katika majimbo mbalimbali nchini ambapo Mgombea urais wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt.John Pombe Magufuli anaongoza  kwa asilimia kubwa katika Majimbo yaliyotajwa, na kuwaacha mbali wapinzani wake, wa tatu kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi (NEC), Dkt. Wilson Mahera na wengine ni Wajumbe wa Tume hiyo, utangazaji Matokeo ya Uchaguzi Mkuu 2020 kwa Kiti cha Urais unafanyika katika Kituo cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), Jijini Dar es Salaam.

Watazamaji wa  Ndani wa Uchaguzi Mkuu 2020 wakifuatilia usomwaji wa  matokea ya Uchaguzi wa Rais,   ambayo yanatangazwa na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC), Mhe. Jaji (Mst), Semistocles Kaijage, katika Kituo cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), Jijini Dar es Salaam.

Mawakala wa Wagombea wa Kiti cha Urais wakifuatilia Matokeo ya Uchaguzi Mkuu 2020 katika kiti hicho ambayo  ambayo yanatangazwa na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC), Mhe. Jaji (Mst), Semistocles Kaijage, katika Kituo cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), Jijini Dar es Salaam.

Waandishi wa Habari wakichukua habari za utangazaji matokeo ambayo yanatangazwa na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC), Mhe. Jaji (Mst), Semistocles Kaijage, katika Kituo cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), Jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC), Mhe. Jaji (Mst), Semistocles Kaijage akitangaza   matokeo ya Uchaguzi wa Rais katika majimbo mbalimbali nchini ambapo Mgombea urais wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt.John Pombe Magufuli anaongoza  kwa asilimia kubwa katika Majimbo yaliyotajwa, kulia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi (NEC), Dkt. Wilson Mahera, utangazaji Matokeo ya Uchaguzi Mkuu 2020 kwa Kiti cha Urais unafanyika katika Kituo cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), Jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC), Mhe. Jaji (Mst), Semistocles Kaijage, akiteta Jambo na Mkurugenzi wa Uchaguzi(NEC), Dkt.Wilson Mahera wakati wa utangazaji matokeo ya Uchaguzi nasfasi ya Urais unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), Jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Uchaguzi (NEC), Dkt.Wilson Mahera akipanga karatasi za matokeo ambayo yamemalizwa kutangazwa na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC), Mhe. Jaji (Mst), Semistocles Kaijage, katika zoezi la utangazaji matokeo ya Uchaguzi wa Rais linalifanyika katika Kituo cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), Jijini Dar es Salaam.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi