Na. Immaculate Makilika
Ualbino ni ukosefu au upungufu wa rangi asili mwilini ambayo huathiri rangi ya ngozi, macho na nywele. Ualbino upo duniani kote na hutokea katika jamii zote, weusi, weupe, na waasia. Aina kuu za ualbino ni ualbino wa macho, ngozi na nywele.
Upungufu huo wa rangi asili mwilini husababisha watu hawa kukumbwa na changamoto mbalimbali ikiwemo za uoni hafifi, ngozi kuathiriwa na mionzi ya jua pamoja na kuwa kwenye hatari ya kutengwa na jamii kwa sababu hali yao haifahamiki na unyanyapaa kuanzia kwenye ngazi ya familia.
L...