Na Mwandishi Wetu, Pwani
WAFANYABIASHARA na wajasiriamali mkoani Pwani wametakiwa kujitokeza kwa wingi kwenye ofisi za Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kwa ajili ya kuthibitisha ubora wa bidhaa wanazozalisha ili kuondokana na vikwazo vya kibiashara ndani na nje ya nchi.
Ushauri huo ulitolewa jana Ofisa Uhusiano wa TBS, Neema Mtemvu, wakati akizungumza washiriki wa Wiki ya Viwanda, Uwekezaji na Biashara mkoani Pwani iliyoanza Oktoba 17, mwaka huu ikitarajiwa kufikia kilele chake Oktoba 23.
Mtemvu, alisema shirika hilo limeshiriki wiki hiyo V...
Read More