Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Uhamiaji Kuwasaka Wahamiaji Haramu Ngorongoro
Jun 22, 2022
Na Jacquiline Mrisho

Na Mwandishi Maalum, Loliondo,

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala ametangaza kuanza kwa operesheni maalum ya siku kumi kusaka wahamiaji haramu katika eneo la Loliondo, Ngorongoro mkoani Arusha.

Kamishna Jenerali Makakala amebainisha hayo leo Loliondo, na kusema kuwa zoezi hilo litaenda sawia na zoezi linaloendelea la uwekaji wa alama za mipaka katika Pori Tengefu la Loliondo.

Dkt. Makakala amesisitiza kufuatwa kwa sheria za nchi pale wageni wanapotaka kuingia au kutoka nchini, na kwamba Uhamiaji imejipanga vema kusimamia eneo hilo katika mipaka yote nchini.

"Nchi yetu imebarikiwa kwa kuwa na maeneo mazuri ambayo yanavutia wahamiaji haramu kufika nchini kwa sababu tofauti, hatutakubali hilo litokee wakati wowote ule," amesema Makakala.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Mwalimu Raymond Mangwala amemfahamisha Dkt.Makakala kuwa Wilaya yake inaendelea vema na utekelezaji wa zoezi la uwekaji wa alama za mipaka katika eneo la Pori Tengefu la Loliondo na kwamba atatoa ushirikiano katika zoezi la kusaka wahamiaji haramu ili wale wote watakaobainika wachukuliwe hatua za kisheria kwa mujibu wa sheria za nchi.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi