Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Mitaa Isiyo na Umeme Handeni Kupata Huduma Hiyo Ifikapo Disemba 2022
Sep 23, 2022
Na Jacquiline Mrisho

Imeelezwa kuwa, Mitaa 28 ambayo bado haina umeme  katika Jimbo la Handeni mjini ipo katika mpango wa kupatiwa umeme kupitia mradi wa umeme vijijini Awamu ya Tatu mzunguko wa Pili unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Hayo yamesemwa  bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Nishati, Wakili Stephen Byabato wakati akijibu swali la Mbunge wa Handeni Mjini, Mheshimiwa Reuben Nhamanilo Kwagilwa ambaye aliuliza kuhusu mpango wa Serikali wa kupeleka umeme katika mitaa 28 ya Jimbo la Handeni Mjini ambayo bado haijapata umeme.

Naibu Waziri alisema kuwa, mitaa hiyo inapelekewa umeme na mkandarasi kampuni ya DERM ELECTRICS TANZANIA ambae yupo katika eneo la kazi na anaendelea na ujenzi wa miundombinu ya umeme katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Handeni.

Naibu Waziri aliongeza kuwa, Jimbo la Handeni Mjini lina jumla ya mitaa 60 ambapo kati ya mitaa hiyo, 32 ina umeme sawa na asilimia 53.3 na mitaa 28 haina umeme sawa asilimia 46.7. 

Alisema kuwa kazi ya kupeleka umeme kwenye mitaa hiyo itakamilika Mwezi Desemba, 2022.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi