Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Kongamano la TEHAMA la Connect to Connect Kufanyika Nchini Septemba
Jul 25, 2022
Na Jacquiline Mrisho

Na Immaculate Makilika – MAELEZO

Mkurugenzi wa Idara ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano kutoka Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mulembwa Munaku amesema kuwa wizara yake kwa kushirikiana na kampuni ya Extensia kutoka nchini Uingereza wamesaini makubaliano ya kuandaa kongamano la TEHAMA litakalofanyika nchini Septemba mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini  Dodoma mara baada ya kusaini makubaliano hayo, Mkurugenzi Munaku amesema kuwa kongamano hilo lilifanyika nchini kwa mara ya kwanza mwaka 2013 na kuendelea hadi mwaka 2015 ambapo wadau kutoka nchini na nje ya nchi walishiriki.

“Mwaka 2016 hadi 2021 kongamano hili lilifanyika katika nchi zingine duniani, mwaka huu Septemba 7 na 8 litafanyika hapa nchini katika jiji la Dar es salaam ambapo tunatarajia takriban washiriki 300 kutoka ndani na nje ya nchi ikiwa ni pamoja na mashirika yanayosimamia mawasiliano Afrika na duniani yatashiriki” anasema Munaku.

Alifafanua “lengo la kongamano hili ni kuongeza matumizi ya Mkongo wa Taifa na kuongeza ubunifu na uwekezaji katika masuala ya TEHAMA ili kuongeza ajira na mapato kwa Serikali sambamba na kutoa fursa kwa watu wengine waje kujifunza nchini”.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa amesema kuwa Mkongo wa Taifa ni nguzo muhimu ya kufikia Tanzania ya Kidijitali ambayo inalenga kuimarisha  mifumo ya utoaji huduma kwa wananchi.

“Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan imejipanga kikamilifu kuimarisha uwekezaji mkubwa ikiwa ni pamoja na kujenga chuo cha TEHAMA nchini”, anasema Msigwa.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi