Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Dkt. Jingu Aongoza Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Taifa ya Sensa ya Watu na Makazi
Sep 27, 2022
Na Jacquiline Mrisho

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu, Dkt. John Jingu ameongoza kikao cha 8 cha Kamati ya Ushauri ya Taifa ya Sensa ya Watu na Makazi kilicholenga kupokea taarifa ya zoezi la Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 iliyofanyika tarehe 23 Agosti, 2022 pamoja na kujadili Rasimu ya Mwongozo wa Matumizi ya Takwimu ya Sensa ya Watu na Makazi nchini.

Kikao hicho kimefanyika leo tarehe 27 Septemba, 2022 katika Ukumbi wa Julius Nyerere Interational Covention Centre Jijini Dar es Salaam (JNICC).

Jukumu kubwa la Kamati hiyo ni kuishauri Kamati Kuu ya Taifa ya Sensa inayoongozwa na Mhe. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar namna bora ya utekelezaji wa masuala ya Sensa.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi