Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Waziri Mulamula Amuaga Balozi wa Ubelgiji Nchini
Jun 27, 2022
Na Jacquiline Mrisho

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Balozi wa Ubelgiji nchini, Mhe. Peter Van Acker katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) ameagana na Balozi wa Ubelgiji nchini, Mhe. Peter Van Acker ambaye amemaliza muda wake wa uwakilishi hapa nchini.

Akizungumza na Mhe. Balozi Peter walipokutana katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam, Waziri Mulamula amesema Tanzania na Ubelgiji zimekuwa na uhusiano wa karibu tangu nchi hiyo ilipofungua Ubalozi wake hapa nchini mwaka 1980.

“Uhusiano kati ya Tanzania na Ubelgiji umekuwa unakuwa na kuimarika kupitia awamu zote za Serikali, tumeshuhudia uwepo wa mipango ya maendeleo katika sekta za maji, elimu, nishati pamoja na biashara na uwekezaji,” amesema Balozi Mulamula.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akimkabidhi  Balozi wa Ubelgiji nchini, Mhe. Peter Van Acker zawadi ya picha

Waziri Mulamula amempongeza Mhe. Balozi kwa kumaliza utumishi wake nchini na kuacha uhusiano kati ya Tanzania na Ubelgiji ukiwa imara.

Balozi Mulamula amesema pamoja na kwamba Balozi Peter anaondoka nchini amemhakikishia kuwa kundi la wafanyabiashara kutoka Ubelgiji litakuja nchini mwaka huu ikiwa ni mwendelezo wa kukuza ushirikiano wa kibiashara na uwekezaji.

Kwa upande wake, Balozi wa Ubelgiji nchini, Mhe. Peter Van Acker ameongelea kuridhishwa kwake na uhusiano uliopo baina ya Ubelgiji na Tanzania na kuahidi kuwa balozi mwema wa Tanzania.

“Nimeishi vizuri hapa Tanzania na nimefurahia kuwa hapa wakati wote wa uwakilishi wangu, kuna mengi ya kujivunia kufanya kazi Tanzania asante sana, amesema Balozi Acker

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi