Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Watendaji Wakuu na Wenyeviti wa Bodi Waaswa Kuzingatia Sheria Kanuni na Taratibu
Nov 02, 2018
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_37716" align="aligncenter" width="900"] Msajili wa Hazina Bw. Athumani Mbuttuka akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina kwa Watendaji Wakuu, Wenyeviti na wajumbe wa Bodi kuhusu usimamizi wa Taasisi na mashirika ya Umma ili kuyawezesha kutimiza malengo ya kuanzishwa kwake.[/caption]

Na: Frank Mvungi- MAELEZO

Msajili wa Hazina Bw. Athumani Selemani Mbuttuka amewata Watendaji wakuu , Wenyeviti na Wajumbe wa Bodi za Taasisi na  mashirika ya umma kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia Sheria, Kanuni, Taratibu na miongozo inayotolewa na Serikali .

Akizungumza katika Semina ya kuwajengea uwezo Viongozi hao, Bw. Athumani amesem,a kuwa lengo la Serikali ni kuona dhamira ya kuazishwa kwa Taasisi na Mashirika ya Umma inafikiwa kwa wakati.

"Kwa mujibu wa vifungu Na.10 (2) (e) na 10 (5) vya Sheria ya Msajili wa Hazina ina mamlaka ya Kusimamia Bodi za Taasisi na Mashirika ya Umma hivyo, tuna wajibu wa kuhakikisha kuwa Bodi na Viongozi wote wanaelewa majukumu yao kwa mujibu  wa sheria, kanuni na taratibu"; Alisisitiza Mbutuka.

[caption id="attachment_37717" align="aligncenter" width="900"] Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania Bw. Edwin Rutageruka akizungumza wakati wa semina kwa Watendaji Wakuu, Wenyeviti na wajumbe wa Bodi kuhusu usimamizi wa Taasisi na mashirika ya Umma ili kuyawezesha kutimiza malengo ya kuanzishwa kwake, Semina hiyo imeandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina.[/caption] [caption id="attachment_37718" align="aligncenter" width="900"] Msajili wa Hazina Bw. Athumani Mbuttuka (katikati)akiwa kwenye picha ya pamoja na sehemu ya watendaji wakuu wa mashirika ya umma walioshiriki katika semina kwa Watendaji hao, Wenyeviti na wajumbe wa Bodi kuhusu usimamizi wa Taasisi na mashirika ya Umma ili kuyawezesha kutimiza malengo ya kuanzishwa kwake.[/caption]

Akifafanua amesema kuwa Bodi  na Watendaji wakuu wanapaswa kuwa makini, wabunifu na kufanya maamuzi sahihi na kwa wakati ili kuhakikisha kuwa Taasisi zinajiwekea mikakati ya kupunguza gharama za uendeshaji zinazotokana na matumizi yasiyo ya lazima hususani safari za Bodi na viongozi zisizokuwa na manufaa kwa Taasisi husika.

Alibainisha kuwa Taasisi zinapaswa kuwa na mikakati madhubuti ya kukusanya mapato ili kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi, sambamba na kuhakikisha kuwa matumizi yote yanafanyika kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na miongozo mbalimbali ya Serikali.

"Taasisi zenye utendaji usioridhisha na zile zinazopata hasara kila mwaka, kuweni wabunifu na kuweka mikakati ya kuboresha utendaji na pia kuhakikisha kuwa, hoja za ukaguzi ( CAG,IAG, TR na PPRA) na maagizo ya kamati za Bunge yawekewa mkakati thabiti na zinatekelezwa ipasavyo na kwa wakati;" Amebainisha Mbutta.

[caption id="attachment_37719" align="aligncenter" width="900"] Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu (MOI) Dkt. Respicius Boniface (kulia) akifuatilia hotuba ya Msajili wa Hazina Bw. Athumani Mbuttuka wakati wa ufunguzi wa semina kwa Watendaji Wakuu, Wenyeviti na wajumbe wa Bodi kuhusu usimamizi wa Taasisi na mashirika ya Umma ili kuyawezesha kutimiza malengo ya kuanzishwa kwake.kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya MOI Prof. Charles Anael Mkonyi.[/caption] [caption id="attachment_37720" align="aligncenter" width="900"] Mwenyekiti wa Bodi ya Prof. Humphrey Moshi akizungumza wakati wa wa semina kwa Watendaji Wakuu, Wenyeviti na wajumbe wa Bodi kuhusu usimamizi wa Taasisi na mashirika ya Umma ili kuyawezesha kutimiza malengo ya kuanzishwa kwake, Semina hiyo imeandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina.[/caption] [caption id="attachment_37721" align="aligncenter" width="900"] Sehemu ya Watendaji wakuu na Wenyeviti na wajumbe wa Bodi wakifuatilia semina ya usimamizi wa Taasisi na mashirika ya Umma ili kuyawezesha kutimiza malengo ya kuanzishwa kwake, Semina hiyo imeandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina.(Picha zote na Frank Mvungi- MAELEZO)[/caption]

Akizungumzia Taasisi zinazopaswa kuchangia asilimia 15 ya mapato ghafi katika mfuko mkuu wa Serikali zinatekeleza wajibu huo kwa mujibu wa sheria kila robo mwaka,Bodi inatakiwa kuhakkisha kuwa, mchango unaowasilishwa ni sahihi na unaendana na kiwango cha mapato ghafi ya Taasisi husika au shirika.

Alisema kuwa upande wa matumizi hasa katika malipo ya posho, marupurupu, na maslahi mbalimbali ya Bodi, Viongozi wa Taasisi na Watumishi yanapaswa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo ya Serikali.

Aliongeza kuwa malipo ya posho za nyumba, posho za simu na umeme yanapaswa kulipwa kwa watumishi wenye stahili hizo kisheria tofauti na ilivyo sasa ambapo baadhi ya Taasisi zinaendakinyume na utaraibu huo.

Pia aliwata Watendaji wakuu na Bodi kutofanya malipo kwa kutumia nyaraka ambazo hazijaidhinishwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina.

Ofisi ya Msajili wa Hazina inafanya kazi kwa ushirikiano ili kujenga Taasisi  zinazoendana na Dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ambazo ni madhubuti, Bora na endelevu kwa maslahi ya wananchi wote na Taifa kwa ujumla.

Ofisi ya Msajili wa Hazina imeratibu mafunzo hayo kwa Watendaji Wakuu, Wenyeviti na Wajumbe wa Bodi za Taasisi na Mashirika ya Umma 17 kwa lengo la kuwajengea uwezo katika utendaji wao wa kusimamia taasisi hizo ili kuongeza ufanisi.

 

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi