Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Waandaaji AFL Wakaribishwa Kufungua Tawi Tanzania
Oct 21, 2023
Waandaaji AFL Wakaribishwa Kufungua Tawi Tanzania
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akisalimiana na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Black Engineering kutoka nchini Italia Massimo Fogliati ambao ndio walioandaa sherehe za Ufunguzi wa African Football League Dar es Salaam.
Na Shamimu Nyaki

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amekutana na kufanya mazungumzo na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Black Engineering kutoka nchini Italia Massimo Fogliati ambao ndio walioandaa  sherehe za  Ufunguzi wa African Football League Dar es Salaam.

Mazungumzo hayo yamefanyika leo Oktoba 21, 2023 jijini Dar  es  Salaam ambapo Mhe. Waziri amewashukuru kwa kufanikisha ufunguzi huo, pamoja na kutoa ajira na fursa  kwa Watanzania ambao walihusika katika ufunguzi huo.

Mhe. Dkt. Ndumbaro amewakaribisha wawekezaji hao kufungua tawi hapa nchini kwakua tayari wana matawi  Saud Arabia na Dubai.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji huyo, Bw. Massimo amepokea pongezi hizo na kushukuru Serikali na Wadau wote wa michezo kwa ushirikiano, ambapo  ameahidi kurudi nchini kwa ajili ya kutafuta fursa zaidi na uwekezaji.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi