Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Trilioni 70 Kuzalisha Gesi Asilia Nchini
Jun 11, 2022
Na Jacquiline Mrisho

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akishuhudia utiaji saini Mkataba wa Awali wa Mradi wa kuchakata na kusindika Gesi Asilia (Liquefied Natural Gas – LNG Project) kwenye Hafla iliyofanyika tarehe 11 Juni 2022 Ikulu, Chamwino Dodoma.

Na Mwandishi Wetu - MAELEZO

Shilingi trilioni 70 zinatarajiwa kutumika kutekeleza mradi wa kusindika na kuchakata gesi asilia (LNG) mkoani Lindi.

Hayo yamesemwa leo Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma na Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba katika hafla ya uwekaji saini wa makubaliano ya awali ya mkataba wa nchi hodhi wa mradi huo.

Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan akizungumza na Viongozi na Wananchi  kwenye Hafla ya utiaji saini Mkataba wa Awali wa Mradi wa kuchakata na kusindika Gesi Asilia (Liquefied Natural Gas – LNG Project) iliyofanyika tarehe 11 Juni 2022 Ikulu, Chamwino Dodoma.

"Utekelezaji wa
Mradi huu unakadiriwa kugharimu zaidi ya Dola za Marekani, Bilioni
thelathini sawa na takribani Shilingi trilioni Sabini," ameeleza Waziri Makamba.

Pamoja na hilo, Mhe. Makamba amezipongeza kampuni za Equinor, Shell na wabia wao kwa
ushirikiano wanaoendelea kuipatia Serikali katika kuhakikisha kuwa mradi
huu unafanyika kwa maslahi ya Taifa na Wawekezaji.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi