Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Tanzania Yashiriki Mkutano wa 26 Kuhusu Mifumo ya Usafirishaji Umeme
Feb 20, 2019
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_40668" align="aligncenter" width="1000"] Timu ya wataalam wa nishati kutoka Tanzania, inayoshiriki katika mkutano unaojadili kuhusu mifumo ya kusafirisha umeme iliyounganishwa katika nchi za Mashariki mwa Afrika (Eastern Africa Power Pool – EAPP), mjini Entebbe, Uganda. Kamishna wa Umeme na Nishati Mbadala, Mhandisi Innocent Luoga (katikati), Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Dkt. Tito Mwinuka (wa pili – kulia), Mhandisi Christopher Bitesigirwe kutoka Wizara ya Nishati (kulia), Mhandisi Meksesius Kalinga kutoka TANESCO (kushoto) pamoja na Mhandisi Pius Gaspar kutoka TANESCO (wa pili - kushoto).[/caption]

Na Veronica Simba – Entebbe

Kamishna wa Umeme na Nishati Mbadala, Mhandisi Innocent Luoga kutoka Wizara ya Nishati, ameongoza timu ya wataalam wa nishati kutoka Tanzania, kushiriki katika mkutano wa 26 wa Kamati Tendaji unaojadili mifumo ya kusafirisha umeme, iliyounganishwa katika nchi zilizopo Mashariki mwa Afrika (Eastern Africa Power Pool – EAPP).

Mkutano huo unaofanyika leo Februari 20, katika mji wa Entebbe nchini Uganda, ni wa ngazi ya wataalam kutoka nchi wanachama ukiwa ni utangulizi wa mkutano wa 14 wa Baraza la Mawaziri wa sekta husika unaotarajiwa kufanyika kesho, Februari 21, 2019.

[caption id="attachment_40669" align="aligncenter" width="1000"] Wataalam wa nishati kutoka nchi wanachama wa Eastern Africa Power Pool (EAPP), wakiwa katika picha ya pamoja, kabla ya kuanza mkutano wao uliojadili masuala mbalimbali kuhusu mifumo ya kusafirisha umeme iliyounganishwa katika nchi husika. Mkutano huo umefanyika Februari 20, 2019 mjini Entebbe, Uganda.[/caption] [caption id="attachment_40670" align="aligncenter" width="1000"] Kamishna wa Umeme na Nishati Mbadala, Mhandisi Innocent Luoga, akiwa katika kikao hicho.[/caption]

Miongoni mwa masuala yanayojadiliwa ni pamoja na maboresho ya mkataba wa ushirikiano kwa nchi wanachama wa EAPP.

Aidha, mkutano unajadili masuala ya biashara ya kuuziana na kusafirisha umeme kupitia mifumo ya EAPP na SAPP (Southern Africa Power Pool)

Nchi wanachama wa EAPP ni Tanzania, Uganda, Kenya, Ethiopia, Libya, Sudan, Misri, Rwanda, DRC na Djibouti.

Mbali na Kamishna Luoga, wataalamu wengine wanaoshiriki mkutano huo kutoka Tanzania ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Dkt. Tito Mwinuka, Mhandisi Christopher Bitesigirwe kutoka Wizara ya Nishati, Mhandisi Meksesius Kalinga kutoka TANESCO pamoja na Mhandisi Pius Gaspar kutoka TANESCO.

Katika mkutano wa 14 wa Baraza la Mawaziri hapo kesho, Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu atamwakilisha Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani.

[caption id="attachment_40671" align="aligncenter" width="1000"] Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Dkt. Tito Mwinuka (wa kwanza – kulia), akiwa katika kikao hicho.[/caption] [caption id="attachment_40672" align="aligncenter" width="927"] Mhandisi Christopher Bitesigirwe kutoka Wizara ya Nishati (kushoto) na Mhandisi Meksesius Kalinga kutoka TANESCO (kulia), wakiwa katika kikao hicho.[/caption]

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi