[caption id="attachment_40668" align="aligncenter" width="1000"] Timu ya wataalam wa nishati kutoka Tanzania, inayoshiriki katika mkutano unaojadili kuhusu mifumo ya kusafirisha umeme iliyounganishwa katika nchi za Mashariki mwa Afrika (Eastern Africa Power Pool – EAPP), mjini Entebbe, Uganda. Kamishna wa Umeme na Nishati Mbadala, Mhandisi Innocent Luoga (katikati), Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Dkt. Tito Mwinuka (wa pili – kulia), Mhandisi Christopher Bitesigirwe kutoka Wizara ya Nishati (kulia), Mhandisi Meksesius Kalinga kutoka TANESCO (kushoto) pamoja na Mhandisi Pius Gaspar kutoka TANESCO (wa pili - kushoto).[/caption]
Na Veronica Simba – Entebbe
Kamishna wa Umeme na Nishati Mbadala, Mhandisi Innocent Luoga kutoka Wizara ya Nishati, ameongoza timu ya wataalam wa nishati kutoka Tanzania, kushiriki katika mkutano wa 26 wa Kamati Tendaji unaojadili mifumo ya kusafirisha umeme, iliyounganishwa katika nchi zilizopo Mashariki mwa Afrika (Eastern Africa Power Pool – EAPP).
Mkutano huo unaofanyika leo Februari 20, katika mji wa Entebbe nchini Uganda, ni wa ngazi ya wataalam kutoka nchi wanachama ukiwa ni utangulizi wa mkutano wa 14 wa Baraza la Mawaziri wa sekta husika unaotarajiwa kufanyika kesho, Februari 21, 2019.
[caption id="attachment_40669" align="aligncenter" width="1000"]Miongoni mwa masuala yanayojadiliwa ni pamoja na maboresho ya mkataba wa ushirikiano kwa nchi wanachama wa EAPP.
Aidha, mkutano unajadili masuala ya biashara ya kuuziana na kusafirisha umeme kupitia mifumo ya EAPP na SAPP (Southern Africa Power Pool)
Nchi wanachama wa EAPP ni Tanzania, Uganda, Kenya, Ethiopia, Libya, Sudan, Misri, Rwanda, DRC na Djibouti.
Mbali na Kamishna Luoga, wataalamu wengine wanaoshiriki mkutano huo kutoka Tanzania ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Dkt. Tito Mwinuka, Mhandisi Christopher Bitesigirwe kutoka Wizara ya Nishati, Mhandisi Meksesius Kalinga kutoka TANESCO pamoja na Mhandisi Pius Gaspar kutoka TANESCO.
Katika mkutano wa 14 wa Baraza la Mawaziri hapo kesho, Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu atamwakilisha Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani.
[caption id="attachment_40671" align="aligncenter" width="1000"]