Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

  Tanzania Yaendelea Kung'ara Kimataifa
Mar 01, 2020
Na Msemaji Mkuu

  [caption id="attachment_51279" align="aligncenter" width="750"] Msemaji mkuu wa Serikali na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbasi[/caption]

Na Mwandishi Wetu

Tanzania imetajwa kuwa nchi ya kwanza Afrika Mashariki na ya nne Afrika kwa kuweka mazingira wezeshi ya ufanyaji biashara ndogondogo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Jijini Dodoma, Msemaji mkuu wa Serikali na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbasi amesema kuwa kidunia Tanzania imeendelea kufanya vizuri katika Nyanja mbalimbali ambapo katika suala hilo anasema kidunia imekuwa ya 21.

“Taasisi za Kimataifa zinatambua juhudi za Serikali yetu katika kuwaletea wananchi maendeleo, Baadhi ya masuala yaliyofanyika kwa wajasiriamali wadogo ni kupewa vitambulisho maalum vya kuwatambulisha, tozo mbalimbali zimefutwa ili kuwesesha ukuaji wa sekta ya biashara hapa nchini”,Alisistiza Dkt. Abbasi

Akifafanua Dkt. Abbasi amesema kuwa Kituo cha Kimataifa cha Televisheni cha CNBC Africa kimerusha makala maalum inayoonesha mafanikio ya Serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo na kuoneshwa na zaidi ya nchi 100 Duniani.

Katika makala hiyo iliyoakisi sekta za utalii, miundombinu, nishati, madini, kilimo na uzalishaji, Dkt. Abbasi amesema kuwa hatua hiyo ni moja ya ishara kuwa Taasisi za Kimataifa zinaendelea kutambua hatua zinazochukiliwa na Serikali ya Awamu ya Tano katika kuwaletea maendeleo wananchi.

Katika hatua nyingine Dkt. Abbasi amesema kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki Prof. Palamagamba Kabudi aliwasilisha ripoti ya Tanzania katika Baraza la Dunia la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu na kusisitiza kuwa Tanzania itaendelea kuheshimu na kulinda haki za binadamu kama ilivyokawaida yake.

“ Haki za Binadamu sio siasa, kama nchi tumeendelea kusisitiza na tutaendelea kuzienzi haki zote za Binadamu kwa maslahi ya watu wote” , alisisitiza Dkt. Abbasi

Tanzania imetajwa kwa nyakati tofauti na Taasisi mbalimbali za Kimataifa kuwa Taifa la kupigiwa mfano kwa namna inavyochukua hatua za kuwaletea wananchi maendeleo, kupiga vita rushwa, kujenga uchumi na ustawi wa wananchi.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi