Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Tanzania na Uganda Zasaini Makubaliano ya Kuboresha Sekta ya Mifugo
Dec 22, 2017
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_25464" align="aligncenter" width="750"] Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Sekta ya Mifugo, Dkt. Mary Mashingo (kulia) akibadilishana nyaraka za makubaliano ya ushirikiano wa kuboresha sekta ya mifugo baina ya Tanzania na Uganda na Mheshimiwa Balozi wa Uganda nchini Tanzania, Bw. Richard Tumusiime Kabonero leo mjini Bukoba.[/caption]

Na John Mapepele

Tanzania  na Uganda leo zimesaini  makubaliano ya kuboresha sekta ya mifugo baina ya nchi mbili kwa kuimarisha ushirikiano katika nyanja za kuthibiti magonjwa hatari ya mlipuko na kuanzisha minada ya  pamoja ya kimataifa kwa maslahi ya nchi zote mbili.

Makubaliano hayo yamesainiwa  kwa upande wa Uganda na Balozi wa Uganda nchini bwana Richard Tumusiime  Kabonero na kwa upande wa Tanzania na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo anayeshughulikia sekta ya Mifugo, Dkt. Mary  Mashingo mjini Bukoba.

Akizungumza mara baada ya utiaji wa saini makubaliano hayo Balozi Kabonero amesema magonjwa ya mlipuko kwa wanyama hayana mipaka hivyo makubaliano yaliyofanyika yatasaidia kudhibiti magonjwa ya wanyama  hatimaye kuboresha  mifugo.

    [caption id="attachment_25465" align="aligncenter" width="750"] Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Sekta ya Mifugo, Dkt. Mary Mashingo (kulia) akitia saini nyaraka za makubaliano ya ushirikiano wa kuboresha sekta ya mifugo baina ya Tanzania na Uganda na Mheshimiwa Balozi wa Uganda nchini Tanzania, bwana Richard Tumusiime Kabonero leo mjini Bukoba. Aliyesimama nyuma (mwenye koti) ni Balozini Suleiman Ahmed saleh, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Afrika, Wizara ya Mambo ya nje aliyesimama kushoto ni Aziz Buwedewo (Picha na John Mapepele).[/caption]

Aidha, amesema  hatua  ya udhibiti wa magonjwa ya mifugo itasaidia kupata mifugo bora itakayokuwa na thamani kubwa katika masoko ya kimataifa na kuingizia  nchi zote  mbili mapato zaidi tofauti na ilivyo sasa ambapo nchi zinapata  hasara kwa kuuza mifugo ikiwa katika kiwango   cha chini.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo anayeshughulikia sekta ya Mifugo, Dkt. Mary  Mashingo amesisitiza kwamba ushirikiano wa kitaalam katika kuratibu,kufuatilia hali ya mifugo na kufanya tathmini ya kila wakati utaleta mafanikio makubwa  baina ya nchi ya Tanzania na Uganda  utaleta mapinduzi  katika sekta badala ya utaratibu wa sasa wa kila nchi kushughulikia  masuala ya peke yake.

“Magonjwa ya mlipuko kwa  wanyama  ni suala mtambuka duniani kote, hivyo ni muhimu kulishughulikia  kwa pamoja ili kuwa na tija” alisisitiza Dkt. Mashingo.

Kwa upande wa himasheria, Dkt. Mashingo amesema kuwa serikali zote zimeangalia namna bora ya kushirikiana utekelezaji wa sheria ili kuwabana wafugaji wasiozingatia sheria  kwenye sekta hiyo.

“Tumeamua kwa pamoja kuanzia sasa  kudhibiti tatizo la utoroshaji wa mifugo kwenye mipaka ya nchi zetu. Hatua kali  zitachukuliwa  ili kutoa fundisho kwa yeyote atakayefanya makosa”

Amesema ili kuboresha masoko  ya mifugo baina ya Uganda na Tanzania wamekubaliana kuwa na minada ya kimataifa katika maeneo ya Mutukula kwa upande wa Tanzania na  Kamwema kwa upande wa Uganda.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji Mifugo na Masoko  kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, bwana Victor Mwita anasema kuwa kuimarika kwa minada itakayosimamiwa kisheria katika mipaka ya nchi ya Tanzania na Uganda itasaidia kuongeza tija katika sekta ya mifugo  hapa nchini.

Aidha, Dkt. Mashingo alisisitiza kwamba wafugaji wenyewe ndiyo wanaoweza kuifanya sekta kupiga hatua kwa kuzingatia  na kusimamia sheria mbalimbali za mifugo nchini. Alizitaja  baadhi ya sheria ambazo ni kipaombele  kwa wafugaji kuzingatia kwa sasa kuwa ni pamoja na Sheria ya Magonjwa ya Mifugo namba 17 ya mwaka 2003 na  Sheria za Nyanda za Malisho na Vyakula vya Mifugo namba 13 ya mwaka 2010.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi