Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Tafiti Zinaonesha Samaki na Dagaa wa Ziwa Victoria Hawajaathirika kwa Zebaki - Dkt. Jafo
Feb 10, 2022
Na Jacquiline Mrisho

Waziri wa Nchin Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Dkt. Selemani Jafo amesema tafiti zinaonesha samaki na dagaa wanaopatikana katika Ziwa Victoria hawajaathirika kwa zebaki.

Amesema hayo bungeni jijinin Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Mhe. Juliana Masaburi aliyetaka kufahamu iwapo Serikali imefanya utafiti kuhusu samaki hao iwapo wameathiriwa na kemikali hiyo kama inavyodaiwa.

Dkt. Jafo alisema kuwa wataalamu wanaendelea kuhakikisha matumizi mbalimbali ya kemikali hiyo katika maeneo ya Kanda ya Ziwa yanadhibitiwa huku akiwataka waendelee kuzingatia masuala mahsusi ya kimazingira ili kulinda nchi yetu.

Pia, akijibu swali kuhusu udhibiti wa uchafuzipembezoni mwa Ziwa Victoria ambao unapunguzasamaki kuzaliana hivyo shughuli za uvuvi kudorora, waziri huyo alisema Serikali imeandaa Kanuni, Miongozo na kuhakikisha Tathmini ya Athari kwa Mazingira (TAM) inafanyika kwa miradi ya maendeleo iliyopo na inayotarajiwa kufanyika pembezoni mwa ziwa hilo.

Aliongeza kuwa imeandaliwa mikakati pamoja na kuendelea kutekeleza katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki kwa ajili ya kubebea bidhaa ambayo kwa kiasi kikubwa ilikuwa ikichangia uchafuzi pembezoni mwa Ziwa Victoria.

Hata hivyo, Dkt. Jafo alibainisha kuwa uchafuzi wa mazingira unaofanyika pembezoni mwa ziwaunatokana na shughuli za kibinadamu zisizozingatia hifadhi ya mazingira zikiwemo utiririshaji wa majitaka kutoka katika maeneo ya makazi pamoja utupaji wa taka ngumu kutoka majumbani na viwandani.

Alitaja shughuli zingine kuwa ni kilimo kisicho endelevu kinachosababisha uchafuzi wa maji kutokana na kuongezeka kwa tabaki (segments) namatumizi yasiyo sahihi ya viuatilifu na mbolea za viwandani na uchimbaji wa madini usio endelevu.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi