Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Taarifa kwa Umma
Oct 12, 2017
Na Msemaji Mkuu

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU

Simu: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: press@ikulu.go.tz Tovuti : www.ikulu.go.tz

Faksi: 255-22-2113425

 
OFISI YA RAIS,       IKULU,  1 BARABARA YA BARACK OBAMA,   11400 DAR ES SALAAM. Tanzania.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 12 Oktoba, 2017 amewasili Zanzibar ambapo keshokutwa tarehe 14 Oktoba atakuwa mgeni rasmi katika sherehe za kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru, Kumbukumbu ya siku ya Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere na kilele cha wiki ya vijana kitaifa zitakazofanyika katika uwanja wa Amaan.

Mhe. Rais Magufuli ambaye ameongozana na mkewe Mama Janeth Magufuli ametua katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume na kupokelewa na Makamu wa Rais wa Pili wa Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Idd.

Jaffar Haniu

Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Zanzibar

12 Oktoba, 2017

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi