Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Taarifa kwa Umma
Mar 28, 2019
Na Msemaji Mkuu

Ikulu, Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Richard Faustine Sambaiga kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Mhe. Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa Dkt. Sambaiga umeanza tarehe 23 Machi, 2019.

Dkt. Sambaiga ni Mhadhiri Mwandamizi, Idara ya Sosholojia ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bi. Rukia Masasi ambaye amemaliza muda wake.

Wakati huohuo, Mhe. Rais Magufuli kesho tarehe 28 Machi, 2019 atamuapisha Mhe.Balozi Mteule Valentino Mlowola kuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba.

Mhe. Balozi Mteule Mlowola ataapishwa Ikulu Jijini Dar es Salaam, kuanzia saa 3:30 asubuhi.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

27 Machi, 2019

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi