Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Taarifa kwa Umma
Feb 27, 2019
Na Msemaji Mkuu

BODI YA WAKURUGENZI YA MAMLAKA YA USIMAMIZI WA WANYAMAPORI TANZANIA – (TAWA)

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Hamisi A. Kigwangalla (Mb.), amekamilisha uteuzi wa safu ya wajumbe wa bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania – (TAWA), kulingana na mamlaka aliyonayo kwa mujibu wa kifungu cha 3.1.1 cha amri ya uanzishwaji wa Mamlaka ya TAWA ( GN na. 135 ya mwaka 2014)  kwa kuwateua wajumbe wengine wawili.

Wajumbe walioteuliwa kukamilisha safu inayotakiwa ni;

  • Jane Claude Mihanji na
  • Bi Magdalena Joseph Kimaty

Uteuzi huu ni wa miaka mitatu kuanzia tarehe 26 Oktoba, 2018.

Wakati huo huo, Waziri wa Maliasili na Utalii, amebatilisha uteuzi wa Dkt. Freddy S. Manongi kuwa mjumbe wa bodi ya TAWA.

Imetolewa na

Dorina G. Makaya

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini

27 Februari, 2019

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi