Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Taarifa kwa Umma
Oct 11, 2018
Na Msemaji Mkuu

Ikulu, Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Dalmas Lucas Nyaoro kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS).

Dkt. Nyaoro ambaye ni Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), anachukua nafasi ya Bi. Hawa Magogo Mmanga ambaye amemaliza muda wake.

Uteuzi wa Dkt. Nyaoro umeanza tarehe 10 Oktoba, 2018.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

11 Oktoba, 2018

 

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi