Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Taarifa kwa Umma
Jun 29, 2018
Na Msemaji Mkuu

Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe Mhe. Emmerson Dambudzo Mnangagwa leo tarehe 29 Juni, 2018 amemaliza ziara yake rasmi ya kiserikali hapa nchini na kurejea nchini kwake Zimbabwe.

Katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam Mhe. Rais Mnangagwa ameagwa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.

Kabla ya kuondoka nchini Mhe. Rais Mnangagwa ametembelea chuo cha kilimo na mifugo cha Kaole kilichopo Bagamoyo Mkoani Pwani ambacho mwaka 1963 kilikuwa kambi ya wapigania uhuru wa chama cha FRELIMO, na yeye akiwa mmoja wa waanzilishi wa kambi hiyo.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

29 Juni, 2018

 

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi