Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Serikali Yawasilisha Muswada wa Kulitangaza Jiji la Dodoma kuwa Makao Makuu ya Nchi
Sep 04, 2018
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_34779" align="aligncenter" width="900"] Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo akiwasilisha Bungeni maelezo ya Serikali kuhusu muswaada wa sheria ya kulitangaza Jiji la Dodoma kuwa makao makuu ya nchi wa mwaka 2018( The Dodoma Capital City ( Declaration) Bill, 2018.[/caption]

Na Jacquiline Mrisho

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR - TAMISEMI), Mhe. Selemani Jafo leo amewasilisha Muswada wa Sheria ya Kulitangaza Jiji la Dodoma kuwa Makao Makuu ya Nchi katika mkutano wa kumi na mbili wa kikao cha kwanza cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Waziri Jafo amesema dhumuni la muswada huo ni kupendekeza kutungwa kwa sheria ambayo italitangaza rasmi Jiji la Dodoma kuwa makao makuu ya nchi na makao makuu ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Waziri Jafo amesema chimbuko la hoja ya kutunga sheria hiyo ni kukosekana kwa sheria inayotambua na kuweka misingi ya uendelezaji wa makao makuu ya nchi, hivyo hatua ya kulitambua jiji la Dodoma kama  makao makuu ya nchi itachochea ukuaji wa mji wa Dodoma na maeneo yanayozunguka mkoa wa Dodoma kiuchumi na kijamii.

“Kukosekana kwa sheria inayotambua Dodoma kuwa makao makuu ya nchi kulisababisha uendelezaji wa makao makuu ya nchi kutofikia malengo, hivyo msingi wa kutunga sheria hii ni kutambua kisheria jiji la Dodoma kuwa makao makuu ya nchi” alisema Waziri Jafo.

Akifafanua kuhusu muswada aliowasilisha mbele ya Spika Job Ndugai, waziri Jafo amesema muswada huo utakuwa na vifungu sita vikiwemo vya utangulizi, matumizi, tafsiri ya maneno yaliyotumika, kulitangaza Jiji la Dodoma kama makao makuu ya nchi na mwisho ni kifungu ambacho kimeweka masharti ya kubadilisha makao makuu ya nchi.

Uamuzi wa kuwasilisha muswada wa kulitanganza jiji la Dodoma kuwa makao makuu ya nchi na serikali ni mwendelezo wa hatua za kimageuzi zinazofanywa na Serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

 

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi