Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Serikali Yawarahisishia Wafanyabiashara Utoaji Risiti za EFD
Nov 08, 2022
Na Jacquiline Mrisho

Na. Haika Mamuya na Farida Ramadhani, WFM, Dodoma

Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imeanzisha mfumo rahisi wa utoaji wa risiti ujulikanao kama Visual Fiscal Devices (VFD) ili kuhakikisha kuwa kila mfanyabiashara anapata mashine za Kutolea Risiti za Kielektroniki (EFD) kwa njia rahisi na isiyo na gharama.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Hamad Hassan Chande alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Mhe. Subira Khamis Mgalu aliyetaka kujua mpango wa Serikali wa kugawa mashine za kutolea risiti EFD kwa Wafanyabiashara ili kuongeza wigo wa walipa kodi.

Mhe. Chande alisema kuwa Mfumo huu wa kisasa wa utoaji wa risiti hauhitaji kutumia mashine kama ilivyo sasa badala yake mtumiaji anaweza kutumia vifaa vingine vya kieletroniki kama vile simu janja, kompyuta na vishikwambi kutoa risiti zilizounganishwa na mfumo wa TRA.

“Mfumo unaendelea kutumika na kusambaa nchi nzima na hauna gharama badala yake mtumiaji ataingia gharama ndogo ya bando ili kupata mtandao wakati wa matumizi”, alifafanua Mhe. Chande.

Aidha, alisema kuwa wafanyabiashara wanaruhusiwa kisheria kujirejeshea gharama ya ununuzi wa mashine za EFD wakati wa uandaaji wa hesabu zao za kodi wanazopaswa kulipa.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi