Na Frank Mvungi- MAELEZO
Serikali ya Awamu yaTano tangu iingie madarakani imefanikisha Ujenzi wa Viwanda zaidi ya 3306 vikubwa na Vidogo hadi kufikia machi 2018.
Akiwasilisha Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi, Waziri wa Viwanda Biashara na uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage amesema kuwa ujenzi wa viwanda hivyo unatokana na dhamira ya Serikali kujenga uchumi wa viwanda ili kukuza ajira na uchumi.
“Muongozo wa Kusimamia ujenzi wa Viwanda kwa Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa umekamilika’’ Alisisitiza Mwijage
Akifafanua Mhe. Mwijage amesema kutokana na dhamira safi ya Serikali kujenga uchumi wa Viwanda hali iliyopelekea Tanzania kujitosheleza kwa mahitaji ya nondo, mabati, vinjwaji na vigae.
Katika kufufua viwanda vilivyosimama kuzalish, Mhe. Mwijage amesema kuwa msimamo wa Serikali nikuhakikisha kiwanda cha matairi Arusha kinafanya kazi na jukumu la kuboresha na kuendesha kiwanda hicho litakuwa mikononi mwa sekta Binafsi huku Serikali ikibaki na hisa kulingana na rasilimali zilizopo.
Akizungumzia vipaumbele vya Wizara kwa mwaka 2018/19 Mhe. Mwijage amesema kuwa ni kuendeleza miradi ya kielelezo ya Mchuchuma na Liganga, Magadi soda Engaruka na Kiwanda cha Matairi Arusha, Uendelezaji wa eneo la Viwanda TAMCO Kibaha na mradi wa kuunganisha matrekta.
Vipaumbele Vingine ni uendelezaji wa Mitaa, Maeneo ya Viwanda vya SIDO, Kuendeleza Kanda Kuu za Kiuchumi, Ruvuma, Tanga, Kigoma, Manyoni, Bagamoyo, SZE na BMSEZ, Kurasini Logistic Centre na Kigamboni Industrial Parks.
Aidha ameongeza kuwa, kati ya Julai 2017 hadi Machi 2018 jumla ya miradi 243 yenye thamani ya dola za kimarekani milioni 3,667 imeajiri watu 36,025 na imesajiliwa na TIC, BRELA na EPZA.
Vilevile amesema kuwa, tangu kuanzishwa kwa Mamlaka ya EPZ hadi mwezi machi, 2018 jumla ya mtaji dola bilioni 1.86 uliwekezwa na mauzo ya bidhaa nje ya nchi yamefikia Dola za Kimarekani milioni 1,359.94 na ajira 52, 698 za moja kwa moja zimepatikana.
Kupitia mradi wa kuunganisha matrekta ya URSUS ambapo hadi mwezi Desemba 2017, Semi knocked Down (SKD) za matrekta 2400 yaliyoanishwa katika mkataba wa uunganishaji unaoendelea.
Pia Wizara itaendeleza tafiti kupitia taasisi zake za TIRDO, CAMARTEC, TEMDO, Dodoma Leather, Dodoma SEZ na ujenzi wa Indusrial Parks.
Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli imekuwa ikisisitiza umuhimu wa ujenzi wa uchumi wa viwanda kote nchini, Aidha Hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2018/2019.