Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Serikali Kuendelea Kuwezesha Wananchi Wanyonge Kumiliki Ardhi
Sep 28, 2018
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_35917" align="aligncenter" width="900"] Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angelina Mabula akihutubia washiriki wa hafla ya uzinduzi wa matokeo ya utafiti wa haki na usalama wa umiliki wa rasilimali ardhi na makazi Tanzania wa mwaka 2017/2018 leo Jijini Dodoma ambapo alizindua taarifa ya utafiti huo .[/caption]

Na Beatrice Lyimo-MAELEZO Dodoma.

Serikali ya Awamu ya Tano itahakikisha wananchi hasa waishio vijijini wanapata haki za msingi za umiliki wa ardhi na makazi nchini.

Hayo yamesemwa leo jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi Mheshimiwa Angelina Mabula wakati wa uzinduzi wa Matokeo ya Utafiti wa Haki na Usalama wa Umiliki wa Rasilimali Ardhi na Makazi Tanzania  mwaka 2017/2018.

"Tunafahamu Watanzania walio wengi na ambao ni masikini wanaishi vijijini na wizara yangu inadhamana ya kusimamia eneo hili, kama Waziri mwenye dhamana nitajitahidi kadri ya uwezo wangu na kuendelea kushirikiana na viongozi wenzangu na wananchi wote kuhakikisha nyaraka rasmi za umiliki ardhi na makazi zinatolewa" ameongeza Dkt. Mabula.

[caption id="attachment_35918" align="aligncenter" width="900"] PIX2. Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi wa matokeo ya utafiti wa haki na usalama wa umiliki wa rasilimali ardhi na makazi Tanzania wa mwaka 2017/2018 leo Jijini Dodoma ambapo alitoa taarifa fupi ya utafiti huo .[/caption]

Aidha, akizungumzia kuhusu utoaji wa hati, Dkt. Mabula amesema kuwa kwa sasa utoaji wa hati umeongezeka kwa mujibu wa taarifa kutoka katika Kanda nane nchini.

"Jumla ya Hati 25,463 zimeandaliwa katika Halmashauri mbalimbali nchini, Hati 17,680 zimewasilishwa ofisi za Kanda kwa ajili ya usajili na Hati 9,739 zimeshakamilika" amefafanua Dkt. Mabula.

hata hivyo Dkt. Mabula amesema kuwa, kwa mwaka 2018/2019 Wizara yake imejipanga kuandaa hati za hakimiliki za kimila 120,000 mpango wa matumizi bora ya ardhi katika vijiji 30 na mpango kina wa vijiji na kupima viwanja 20,000 ikiwa ni kumuwezesha mwananchi kuwa na uhakika na salama ya miliki yake na kuepusha mgogoro.

[caption id="attachment_35919" align="aligncenter" width="750"] Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angelina Mabula akikata utepe kuzinduzi wa matokeo ya utafiti wa haki na usalama wa umiliki wa rasilimali ardhi na makazi Tanzania wa mwaka 2017/2018 leo Jijini Dodoma.[/caption]

Nae Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa amesema kuwa utafiti huo umelenga kutoa viashiria mbalimbali kuhusu rasilimali ardhi, nyumba na makazi nchini na kutumika katika kufuatilia malengo yaliyopo katika Mpango kazi wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano ijayo, Malengo endelevu ya Maendeleo na Afrika Ajenda 2063.

"Utafiti huu ulifanyika Tanzania Bara na Zanzibar na sampuli ilichaguliwa kwa utaalamu na ilitumika kwa watu wazima wenye umri wa miaka 18 na kuendelea" ameongeza Dkt. Chuwa.

Utafiti wa Haki na Usalama wa Umiliki wa Rasilimali Ardhi na Makazi Tanzania kwa mara ya kwanza ulifanyika mwaka 2016/2017 na wa pili mwaka 2017/2018 na watatu mwaka 2018/2019 unaendelea na ukusanyaji wa taarifa za kitakwimu ambao matokeo yake yatazinduliwa mwaka 2019

[caption id="attachment_35920" align="aligncenter" width="900"] Sehemu ya washiriki wa hafla uzinduzi wa matokeo ya utafiti wa haki na usalama wa umiliki wa rasilimali ardhi na makazi Tanzania wa mwaka 2017/2018 leo Jijini Dodoma, Utafiti huo umezinduliwa na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angelina Mabula.[/caption] [caption id="attachment_35921" align="aligncenter" width="900"] Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angelina Mabula akimkabidhi Kamishna wa Ardhi Msaidizi Kanda ya Kati Bw. Ezekiel Kitilya matokeo ya utafiti wa haki na usalama wa umiliki wa rasilimali ardhi na makazi Tanzania wa mwaka 2017/2018 leo Jijini Dodoma.[/caption] [caption id="attachment_35922" align="aligncenter" width="900"] Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bw. akizungumza wakati wa hafla ya kuzindua matokeo ya utafiti wa haki na usalama wa umiliki wa rasilimali ardhi na makazi Tanzania wa mwaka 2017/2018 leo Jijini Dodoma.[/caption] [caption id="attachment_35923" align="aligncenter" width="900"] Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angelina Mabula akionesha matokeo ya utafiti wa haki na usalama wa umiliki wa rasilimali ardhi na makazi Tanzania wa mwaka 2017/2018 leo Jijini Dodoma wakati wa hafla ya uzinduzi wa matokeo ya utafiti huo.[/caption] [caption id="attachment_35924" align="aligncenter" width="900"] Mwakilishi wa Shirika la Global Land Allience ya Marekani inayojishughulisha na masuala ya haki miliki ya Ardhi na Makazi Dkt. David Ameyaur akizungumzia faida za matokeo ya utafiti wa haki na usalama wa umiliki wa rasilimali ardhi na makazi Tanzania wa mwaka 2017/2018 leo Jijini Dodoma wakati wa uzinduzi wa matokeo ya utafiti huo.[/caption]

(Picha zote na Frank Mvungi- MAELEZO, Dodoma)

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi