Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Serikali Inawathamini Wawekezaji Sekta ya Michezo
Jun 28, 2019
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_44714" align="aligncenter" width="1000"] Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe (Katikati) akizungumza na wanafunzi (hawapo katika picha) ambao pia ni wanamichezo wa Shule ya Sekondari ya Foutain Gate Academy leo Juni 28,2019 alipofanya ziara kituoni hapo kuona namna vijana hao wanavyofundishwa michezo mbalimbali.Kushoto ni Meneja wa kituo hicho Bw.Wendo Makau, na kulia ni Mkuu wa Shule ya Msingi Bw.William Tumshabe.[/caption]

Na Shamimu Nyaki -WHUSM

Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe amesema kuwa Serikali inatambua na kuthamini mchango mkubwa unaofanywa na Taasisi pamoja na vituo vya kukuza vipaji katika sekta ya michezo hapa nchini kwakua imechangia kwa kiasi kikubwa kupatikana kwa wachezaji wengi walioliwakilisha Taifa vizuri katika mashindano mbalimbali.

Waziri Mwakyembe ameyasema hayo leo, Jijini Dododma alipotembelea kituo cha mafunzo ya Michezo cha Foutain Gate Academy ambapo mbali na kuupongeza uongozi wa kituo hicho na kuahidi kutafuta wafadhili mbalimbali watakaowezesha kituo hicho kufanya vizuri zaidi.

"Mnafanya kazi kubwa sana ya kuibua na kukuza vipaji, nawaahidi Serikali itaendelea kushirikiana nanyi pale ambapo mtakwama ikiwemo kutuma timu ya Wataalam wa michezo kutoka Wizarani ili waje kutoa ushauri wa kitaalam katika michezo pamoja na kupokea maoni kutoka kwenu ili kwa pamoja tukuze sekta ya michezo"Dkt Mwakyembe.

[caption id="attachment_44715" align="aligncenter" width="875"] Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Foutain Gate Academy Bw.Dennis Joel akizungumza leo Jijini Dodoma wakati Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe (kulia) alipofanya ziara kituoni hapo kuona namna vijana hao wanavyofundishwa michezo mbalimbali.[/caption] [caption id="attachment_44716" align="aligncenter" width="893"] Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akiongozwa na uongozi wa Sekondari ya Foutain Gate Academy kukagua uwanja wa mpira wa shule hiyo leo Juni 28,2019 Jijini Dodoma alipofanya ziara shuleni hapo kuona namna vijana hao wanavyofundishwa michezo mbalimbali.[/caption] [caption id="attachment_44717" align="aligncenter" width="1000"] Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe akiangalia makombe ambayo Shule ya Sekondari ya Foutain Gate Academy wameshawahi kuyapata katika mashindano mbalimbali leo Juni 28,2019 alipofanya ziara kituoni hapo kuona namna vijana hao wanavyofundishwa Michezo mbalimbali.[/caption] [caption id="attachment_44718" align="aligncenter" width="1000"] Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe akiangalia makombe ambayo Shule ya Sekondari ya Foutain Gate Academy wameshawahi kuyapata katika mashindano mbalimbali leo Juni 28,2019 alipofanya ziara kituoni hapo kuona namna vijana hao wanavyofundishwa Michezo mbalimbali.[/caption]  

Aidha,  Dkt.Mwakyembe ameiagiza Idara ya Maendeleo ya Michezo kufika katika kituo hicho kuona namna mafunzo yanavyoendeshwa pamoja na kutoa elimu kuhusu taaluma za Michezo zinazotolewa na Chuo cha Michezo cha Malya ili wakufunzi wa kituo hicho waweze kwenda kujifunza zaidi katika chuo hicho.

Naye Mkuu wa Shule ya Sekondari hiyo Bw,Dennis Joel amesema kuwa shule hiyo mbali na kutoa elimu,imeweka Michezo kipaumbele ili kupata vijana wengi wasomi lakini pia wanaoweza kucheza michezo mbalimbali ambayo inaweza kuwapatia ajira.

Kwa upande wake Meneja wa Kituo hicho Bw.Wendo Makau amesema kituo hicho kinalengo la kukuza vipaji na kuwaandaa vijana watakaoshiriki michezo nje ya nchi kwakua vijana wengi wana ndoto ya kufikia hatua ya kucheza nje ya nchi.

Naye Nahodha wa timu ya mpira wa miguu chini ya umri wa miaka 20 Ramadhan Albert amesema anashukuru nafasi aliyoapata ya kujiunga na kituo hicho kwakua ndoto zake ni kuwa mwanamichezo mkubwa ndani na nje ya nchi.

   

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi