Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

RC Rukwa Ahimiza Halmashauri Kutumia Mashine za EFD Kuongeza Mapato.
Nov 16, 2017
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_22689" align="aligncenter" width="750"]
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akitoa maelekezo kwa Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga juu ya kuzidisha juhudi za kukusanya mapato.[/caption]
Na.Mwandishi Wetu, Rukwa.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amezihimiza Halmashauri zote Mkoani humo kuhakikisha zinaongeza idadi ya mashine za EFD ili kuongeza ukusanyaji wa mapato yao katika Halmashauri.

Amesema kuwa kwa mwaka wa fedha 2016/2017 Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ilikisia kukusanya Shilingi bilioni 2.3 ambapo hadi sasa Wilaya imekusanya Shilingi bilioni 1.9 ikiwa ni ongezeko la asilimia 97 katika makusanyo ya ndani ya Halmashauri hiyo.

“Halmashauri Ziongeze hizo mashine, kama mnavyofahamu serikali hii inahimiza ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa kutumia mfumo wa Kielektroniki, wenyewe mmekuwa mashuhuda mmevuka kile kiwango mlichojiwekea na kupata ongezeko la asilimi 97 kama mlivyosoma kwenye taarifa yenu, mkiongeza mashine hizo zikafikia idadi inayotakiwa makusanyo ya ndani yatakuwa mengi zaidi,” Alieleza.

Ameongeza kuwa makusanyo ya ndani yakiwa mengi zaidi itasababisha shughuli za kimaendeleo kufanyika kwa wingi zaidi, ikiwemo ujenzi wa vyumba vya madarasa, huku upungufu wa vyumba hivyo ukiwa ni 1399.

Ameyasema hayo baada ya kusomewa taarifa ya Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga katika Ziara yake ya siku mbili yenye lengo la kutembelea miradi mbalimbali, kujitambulisha kwa watumishi pamoja na kuongea na makundi mbalimbali ya wananchi katika halmashauri hiyo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa H/W ya Sumbawanga John Msemakweli amesema kuwa hadi sasa Halmashauri ina mashine za Kielektroniki 64 na uhitaji ni mashine 114 na kusababisha upungufu wa mashine 50 huku akiahidi kuzikamilisha ili kuweza kuongeza mapato ya Halmashauri hiyo.

“Tuna upungufu wa vyumba vya madarasa 1399 na hadi sasa kwa mpango wa kujenga vyumba vitatu kwa kila shule tuna vyumba 98 ambavyo vipo usawa wa linta na kwengine tunaendelea kuwahamasisha wananchi kuweza kuchangia katika ujenzi,” Alisema.

Mkuu wa Mkoa pia aliziagiza Halmashauri  kuangalia upya mpango wao wa ujenzi wa madarasa hayo kwani itawachukua muda mrefu ikiwa watajenga madarasa 98 kwa mwaka.
         

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi