Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Rais Magufuli Amteua CPD
May 23, 2019
Na Msemaji Mkuu

Ikulu, Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Bw. Onorius John Njole kuwa Mwandishi Mkuu wa Sheria (Chief Parliamentary Draftsman – CPD).

Uteuzi wa Bw. Njole umeanza leo tarehe 23 Mei, 2019.

Kabla ya uteuzi huo, Bw. Njole alikuwa Mkurugenzi wa Sheria na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA).

Bw. Njole anachukua nafasi ya Bi. Sara K. Barahomoka ambaye anastaafu.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

23 Mei, 2019

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi