Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Rais Dkt. Magufuli Amteua Mhe. Benjamin Mkapa kuwa Mkuu wa Chuo cha UDOM
May 14, 2019
Na Msemaji Mkuu

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Ikulu, Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Mhe. Benjamin William Mkapa (Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Mhe. Mkapa ameteuliwa kushika wadhifa huo kwa kipindi cha pili mfululizo.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amemteua Prof. Ignas Aloys Rubaratuka kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA).

Prof. Rubaratuka ameteuliwa kushika wadhifa huo kwa kipindi cha pili mfululizo.

Uteuzi wa viongozi hao umeanza tarehe 10 Mei, 2019.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

14 Mei, 2019

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi