Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Naibu Waziri Mabula : Ongezeni Juhudi Ukusanyaji wa Kodi Pango la Ardhi.
Nov 03, 2017
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_21660" align="aligncenter" width="750"] Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angelina Mabula akipata maelezo kutoka kwa Afisa Ardhi wa Manispaa ya Ubungo Bi. Saada Rashid kuhusu mfumo mpya wa ukusanyaji kodi ya pango la ardhi mapema leo alipotembelea katika kituo hicho cha ukusanyaji kodi kwa njia ya kielektroniki katika ziara yake ya kikazi Jijini Dar es Salaam.[/caption]

Na. Paschal Dotto

Serikali imezitaka Halmashauri nchini kuimarisha ukusanyaji kodi hususani katika pango la ardhi na kuachana na kodi ndogondogo ili kuweza kujiendesha zenyewe katika shughuli mbalimbali za maendeleo.

Akizungumza na watumishi wa Manispaa ya Ubungo Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angelina Mabula alisema kuwa katika mfumo mpyawa kielekitroniki ambao kwa sasa umewekwa katika Idara ya ardhi kwa lengo la kodi ya pango la ardhi, ni mfumo rahisi kwa Manispaa zote nchini.

[caption id="attachment_21661" align="aligncenter" width="750"] Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angelina Mabula akitoa maelekezo kwa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Bw. Kisare Makori (katikati) kuhusu utunzaji wa mafaili ya utoaji hati za ardhi alipotembelea Masjala ya Manispaa hiyo katika ziara yake ya kukagua mfumo mpya wa ukusanyaji kodi ya pango la ardhi, kutoka kulia ni Maafisa Ardhi wa Manispaa hiyo.[/caption] [caption id="attachment_21662" align="aligncenter" width="750"] Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Bw. Kisare Makori akimkaribisha katika ofisi za Wilaya hiyo Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angelina Mabula mara baada ya kutembelea ofisi za ukusanyaji wa kodi ya pango la ardhi kwa njia ya kielekroniki na Masjala ya Manispaa hiyo leo Jijini Dar es Salaam.[/caption]

Katika ziara yake ya kikazi inayoendelea katika Mkoa wa  Dar es Salaam Waziri Mabula aliwataka watendaji wa Manispaa hiyo kuhakikisha wadaiwa sugu wapatao 300 wanafuatiliwa na kulipa madeni yao ili kuongeza mapato yatakayosaidia kuendesha shughuli za manispaa ikiwemo kulipa mishahara ya watumishi, kulipa fidia kwa maeneo  wanayohitaji kuyatwaa kwa shughuli za Manispaa.

“Bajeti yenu ni ndogo ukilinganisha na wadaiwa sugu kwa Manispaa yenu mnawadai milioni 500 kwa block ya kimara tu, mnaviwanja 2,1210 kwa hiyo mkidai kwa Manispaa nzima mnaweza kupata pesa nyingi ambayo itawezesha shughuli za Halmashauri kusonga mbele”, alisema Mhe. Mabula.

Mhe. Mabula aliwataka kuimarisha  zaidi katika kusimamia masharti ya utoaji hati na kuwachukulia hatua watu waliojenga ovyo bila vibali vya ujenzi na kuwasihi waanze kuwasaka.

[caption id="attachment_21663" align="aligncenter" width="750"] Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Bw. Kisare Makori (kushoto) akieleza jambo kwa watumishi wa Manispaa hiyo wakati wa kikao kazi na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angelina Mabula (wa tatu kulia) alipotembelea kukagua mfumo mpya wa ukusanyaji pango la ardhi leo Jijini Dar es Salaam, kutoka kulia ni Diwani wa Kata ya Kibamba Ernest Mgawe na wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Manispaa hiyo John Kayombo.[/caption] [caption id="attachment_21664" align="aligncenter" width="750"] Kaimu Mkurugenzi Urasimishaji Makazi kutoka Wizara ya ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bi. Beritha Mlonda akitoa maelezo kwa watumishi wa Manispaa ya Ubungo kuhusu urasimishajia makazi na ujenzi wa huduma za jamii katika maeneo yanayomilikiwa na wananchi wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angelina Mabula leo Jijini Dar es Salaam.[/caption]

“Fedha zote ziko kwenye Idara hii ya ardhi kiasi kwamba mkiweza kusimamia zoezi la ukusanyaji pango la ardhi na utoaji wa hati kwa kufuata utaratibu sahihi, fedha hiyo ingeweza kuleta mapato mengi sana”, alisisitiza Mhe. Mabula.

Aidha Naibu Waziri Mabula aliwataka watendaji wa Manispaa hiyo kuhuisha Mabaraza ya Ardhi ya Kata na kuwapa elimu kuhusu masuala ya migogoro ya ardhi, ambapo pia aliwashukuru kwa kuweza kutatua migogoro 37 ya ardhi katika Manispaa ya Ubungo kiasi ambacho wanaonyesha kuwa na mwelekeo katika kutatua migogoro ya ardhi  kwa haraka.

[caption id="attachment_21665" align="aligncenter" width="750"] Mkurugenzi Msaidizi Kitengo cha Upimaji Vijijini Bw. Huruma Lugala akitoa ufafanuzi wa maeneo ya mipaka kwa Wilaya ya Ubungo, Ilala na Kisarawe hoja iliibuliwa na watumishi wa Manispaa ya Ubungo katika ziara ya Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angelina Mabula katika Manispaa hiyo Jijini Dar es Salaam. (Picha na Paschal Dotto).[/caption]

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa  ya Ubungo Bw. John Kayombo alibainisha Upungufu wa Watumishi katika Idara ya ardhi ambapo aliiomba Serikali  kuwapatia watumishi ili kukidhi mahitaji na kurahisha ufanisi wa kazi katika Manispaa hiyo.

Aliongeza kuwa Serikali itoe suluhu katika migogoro ya mipaka kwa Wilaya hiyo ili kuwezesha upatikanaji wa maeneo ya kutengeneza fursa kwa wa wakazi wa Manispaa ya Ubungo.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi