Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Mkutano Maalum wa Baraza la Vyama Vyama vya Siasa Kufanyika Agosti 28 hadi 30 Jijini Dar es Salaam
Aug 16, 2023
Mkutano Maalum wa Baraza la Vyama Vyama vya Siasa Kufanyika Agosti 28 hadi 30 Jijini Dar es Salaam
Mwenyekiti wa  Baraza la Vyama vya Siasa, Ndg. Juma Ali Khatib akisoma maazimio yatokanayo na mkutano wa Baraza hilo uliofanyika tarehe 1 Agosti, 2023 jijini Dar es Salaam mbele ya Waandishi wa Habari mara baada ya kumaliza Kikao cha Kamati ya Uongozi wa Baraza hilo leo tarehe 16 Agosti, 2023 jijini Dodoma. Kikao hicho kilichokuwa na ajenda ya kupitia maazimio hayo na maandalizi ya Mkutano Maalum wa Baraza hilo unaotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 28 hadi 30 Agosti, 2023. Kulia ni Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa, Mohamed Ali Ahmed na Msajili Msaidizi Sisty Nyahoza.
Na Mwandishi Wetu

Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili na Uhusiano ya Baraza la Vyama vya Siasa, Ndg. Doyo Hassan Doyo akichangia mada wakati wa kikao cha Kamati ya Uongozi ya Baraza la Vyama vya Siasa kilichofanyika leo tarehe 16 Agosti ,2023 jijini Dodoma. Kikao hicho kilikuwa na ajenda ya kupitia maazimio hayo na maandalizi ya Mkutano Maalum wa Baraza hilo unaotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 28 hadi 30 Agosti, 2023. Kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Masuala ya Bunge na Siasa, Ndg. Abdul Mluya na kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili na Uhusiano, Ndg. Mohamed Omari Shaame.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Sheria na Utawala Bora ya Baraza la Vyama vya Siasa, Ndg. Rashid Mohamed Rai akichangia mada wakati wa kikao cha Kamati ya Uongozi ya Baraza la Vyama vya Siasa kilichofanyika leo tarehe 16 Agosti 2023 jijini Dodoma.

 

Wajumbe wa Kamati ya Uongozi wa Baraza la Vyama vya Siasa nchini Tanzania wakiongozwa na Mwenyekiti wa Baraza hilo, Ndg. Juma Ali Khatib (aliyevaa tai) wakiwasilisha maazimio ya Mkutano wa Baraza la Vyama vya Siasa uliofanyika tarehe 1 Agosti, 2023 mbele ya Waandishi wa Habari mara baada ya kumaliza Kikao cha Kamati ya Uongozi wa Baraza hilo leo tarehe 16 Agosti, 2023 jijini Dodoma.

 

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi