Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Mgodi wa ZEM Wapewa Siku Saba Kutoa Vifaa vya Kujikinga
Dec 29, 2017
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_25857" align="aligncenter" width="750"] Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (wa pili kushoto) akitembelea Mgodi wa Dhahabu wa ZEM Tanzania Company Limited alipofanya ziara mgodini hapo kujionea shughuli ziazoendelea. wa pili kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Butiama Annarose Nyamubi.[/caption]

Serikali imetoa siku Saba kwa Mgodi wa Dhahabu wa ZEM (T) Company Ltd wa Nyasirori Wilayani Butiama kuwapatia vifaa vya kujikinga kazini wafanyakazi wa mgodi huo vinginevyo mgodi utafungwa.

Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo ametoa agizo hilo Desemba 27, 2017 alipofanya ziara kwenye mgodi huo kujionea shughuli zinazoendelea mgodini hapo na kuzungumza na wafanyakazi na wananchi wanaozunguka maeneo jirani na mgodi huo.

Wafanyakazi na wananchi wanaozunguka mgodi huo walimueleza Naibu Waziri huyo changamoto mbalimbali walizonazo kutokana na shughuli za mgodi ikiwemo mahusiano mabaya na wananchi, wafanyakazi kukosa vifaa vya kujikinga, mishahara midogo na manyanyaso ikiwemo kupigwa.

Akitoa tamko kuhusiana na hoja hizo zilizowasilishwa kwake, Naibu Waziri Nyongo aliuagiza mgodi huo kufanya shughuli zake kwa kufuata utaratibu, kanuni na sheria za nchi.

[caption id="attachment_25858" align="aligncenter" width="750"] Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (kushoto) akitoa maelekezo kwa Mgodi wa Dhahabu wa ZEM Tanzania Company Limited alipofanya ziara mgodini hapo kujionea shughuli ziazoendelea na kuzungumza na wafanyakazi na wananchi wanaozunguka mgodi huo. Kulia ni Meneja wa Mgodi, Luo Guiquan.[/caption]

Alisema haiwezekani wafanyakazi wakafanya shughuli mgodini hapo bila kuwa na vifaa vya kujikinga na aliiagiza Ofisi ya Madini Musoma kufuatilia suala hilo na endapo siku hizo zitapita bila vifaa hivyo kuletwa afunge mgodi.

“Ninawapa Siku Saba wawe wameleta vifaa na wasipofanya hivyo mgodi utafungwa, ni lazima wafanyakazi wapatiwe vifaa vya kujikinga, kulingana na kazi wanazofanya,” alisema Nyongo.

Akizungumzia suala la mishahara, Naibu Waziri Nyongo aliuagiza mgodi huo kuhakikisha unafuata Sheria ya Madini inavyoelekeza kwa kuwalipa mshahara stahiki ambao alisema kima cha chini kuwa ni 400,000.

Naibu Waziri Nyongo vilevile aliuagiza mgodi huo kuandaa mikataba ya ajira na kwamba atakapofanya tena ziara mgodini hapo akute wafanyakazi wanayo mikataba ya ajira iliyoandaliwa kwa mujibu wa sheria.

[caption id="attachment_25860" align="aligncenter" width="750"] Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Nyasirori Wilaya ya Butiama, Mkoani Mara wakimsikiliza Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (hayupo pichani) alipofanya ziara kwenye Mgodi wa Dhahabu wa ZEM Tanzania Company Limited uliopo katika kijiji hicho.[/caption]

Aidha, aliuonya mgodi huo tabia ya kupiga wafanyakazi, alisema jambo hilo halikubaliki na ni kinyume na utu wa binaadamu na kwamba ikitokea mfanyakazi akapigwa, Ofisi ya Madini ifunge mgodi huo mara moja.

“Ni marufuku kupiga wafanyakazi, atakayepigwa aende Polisi na sisi tutaufunga mgodi. Mkuu wa Wilaya yupo hapa muwe mnamueleza matatizo yenu ili yapatiwe ufumbuzi,” alisema Naibu Waziri Nyongo.

Alimuagiza Mkuu wa Wilaya ya Butiama kusimamia vyema masuala yote ya ulinzi na usalama, na ahakikishe anatembelea mgodini hapo ili kuzungumza na wafanyakazi katika kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili.

[caption id="attachment_25861" align="aligncenter" width="750"] Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (katikati) akizungumza na wafanyakazi wa Mgodi wa Dhahabu wa ZEM Tanzania Company Limited uliopo Butiama, Mkoani Mara (hawapo pichani) wakati wa ziara yake mgodini hapo. Kushoto ni Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji Wadogo wa Madini Tanzania (FEMATA), John Bina.[/caption]

Vilevile Naibu Waziri Nyongo aliuagiza mgodi huo kutofukuza mfanyakazi yoyote aliyeeleza changamoto zinazowakabili kwenye utekelezaji wa majukumu yao. “Usimfukuze mfanyakazi yoyote aliyetoa kero yake katika ziara hii, wako huru kuzungumza nami,” alionya Naibu Waziri Nyongo.

Kuhusu suala la mahusiano na wananchi, Nyongo aliuagiza mgodi huo kuajiri mtu maalum wa mahusiano atakayefanya mawasiliano ya mara kwa mara na wananchi ili kuboresha mahusiano na hapohapo aliiagiza Serikali ya Kijiji kufanya mikutano ya mara kwa mara na wanachi ili kuwapatia mrejesho wa masuala mbalimbali baina ya mgodi na maendeleo ya kijiji.

 

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi