Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Matukio Katika Picha Ziara ya TAGCO Halmashauri ya Wilaya ya Bahi
Sep 02, 2018
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_34687" align="aligncenter" width="750"] Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Bibi. Rachel Chuwa akizungumza katika kikao baina yake na viongozi wa Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Seriikalini (TAGCO) na Idara ya Habari –MAELEZO wakati wa ziara ya kutembelea Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri za Kanda ya Kati jana Mkoani Dodoma. Kutoka kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa TAGCO, Bi. Sarah Kibonde Msika,Mjumbe wa Kamati Tendaji wa TAGCO, Inocent Byarugaba, Afisa Habari wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Benton Nolo na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari –MAELEZO, Bi. Zamaradi Kawawa.[/caption] [caption id="attachment_34688" align="aligncenter" width="1000"] Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari –MAELEZO,Bi. Zamaradi Kawawa akimwelezea jambo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Bibi Rachel Chuwa (kulia) wakati wa ziara ya kutembelea Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri za Kanda ya Kati jana mkoani Dodoma. Kutoka kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa TAGCO, Bi. Sarah Kibonde Msika, Mweka Hazina Msaidizi wa TAGCO, Gerald Chami na Afisa Habari wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Benton Nolo.[/caption] [caption id="attachment_34689" align="aligncenter" width="1000"] Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari –MAELEZO,Bi. Zamaradi Kawawa akiagana na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Bibi Rachel Chuwa (kulia) mara baada ya kumaliza mazungumzo wakati wa ziara ya kutembelea Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri za Kanda ya Kati katika Ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma jana.[/caption] [caption id="attachment_34690" align="aligncenter" width="1000"] Afisa Habari wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Benton Nolo (kushoto) akisindikiza ujumbe wa Viongozi wa Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini walioambatana na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari –MAELEZO anayeshughulikia Uratibu wa Vitengo vya Mawasiliano Serikalini, Bibi. Zamaradi Kawawa (kulia) mara baada ya kukamilisha ziara yao katika wilayani Bahi jana. Viongozi hao wapo katika ziara ya kutembelea Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri nchini kwa lengo la kujionea changamoto zinazowakabili. (Picha na: Idara ya Habari – MAELEZO, Bahi).[/caption]

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi