Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Matukio Katika Picha Uzinduzi wa Tume ya Madini
May 31, 2018
Na Msemaji Mkuu

Waziri wa Madini Mhe. Angellah Kairuki  (Mb) akihutubia washiriki wa hafla ya uzinduzi wa Tume ya Madini  Jijini Dodoma ambapo alikuwa mgeni rasmi .

Mwenyekiti wa Tume ya Madini Prof. Idrissa   Kikula  akihutubia  washiriki wa wa hafla ya uzinduzi wa Tume ya Madini  Jijini Dodoma ambapo Waziri wa Madini Mhe. Angellah Kairuki  (Mb)   alikuwa mgeni rasmi .

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge  akisisitiza kuhusu fursa zilizopo Mkoani Dodoma wakati  wa  wa hafla ya uzinduzi wa Tume ya Madini  Jijini Dodoma.

Mwenyekiti wa  Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Mhe. Dustan Kitandula akizungumzia  manufaa ya kuanzishwa kwa Tume ya Madini wakati wa  hafla ya uzinduzi wa Tume hiyo  Jijini Dodoma

Katibu Mkuu Wizara ya Madini Prof. Simon Msanjila  akitoa hotuba ya kumkaribisha Waziri wa Madini Mhe. Anjellah Kairuki Kuzindua Tume ya Madini leo Jijini Dodoma.

Waziri wa Madini Mhe. Angellah Kairuki  (Mb) akifurahia jambo na   Mwenyekiti wa Tume ya Madini Prof. Idrissa   Kikula wakati akimkabidhi vitendea kazi mara baada ya Kuzindua Tume hiyo leo Jijini Dodoma.

Waziri wa Madini Mhe. Angellah Kairuki  (Mb) akimkabidhi vitendea kazi  Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume hiyo Prof.   Shukrani Manya  mara baada  ya Kuzindua Tume hiyo leo Jijini Dodoma.

Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Prof. Florens  Luoga   ( kushoto) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Dkt. Aderladus Kilangi(  kulia)  Wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Madini  ambaye alikuwa mgeni rasmi wakati wa  hafla ya uzinduzi wa Tume ya madini  leo Jijini Dodoma.

Makamishana wa Tume hiyo wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Madini Mhe. Angellah Kairuki  (Mb) ambaye alikuwa mgeni rasmi wakati wa hafla ya kuzindua Tume hiyo leo Jijini Dodoma.

Waziri wa Madini Mhe. Angellah Kairuki  (Mb) akimkabidhi  Vitendea kazi  mmoja wa Makamishna wa Tume hiyo Dkt. Florence  Turuka ambaye pia ni  Katibu Mkuu Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa wakati wa hafla ya uzinduzi wa Tume ya Madini leo Jijini Dodoma.

Waziri wa Madini Mhe. Angellah Kairuki  (Mb) akiwa kwenye picha ya pamoja na Makamishna wa Tume ya Madini mara baada ya Kuzindua Tume hiyo leo Jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Madini Mhe. Dotto Biteko (kushoto) akiteta jambo na Waziri wa Madini Mhe. Anjellah Kairuki wakati wa hafla ya kuzindua  Tume hiyo iliyofanyika leo Jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt. Anjelina Mabula  akiteta jambo na Naibu Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Elias Kuandikwa wakati wa hafla ya uzinduzi wa Tume ya Madini leo Jijini Dodoma.

 ( Picha zote na Frank Mvungi )

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi