Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Matukio Katika Picha Mafunzo Ya Uandishi wa Habari za Kitakwimu
May 26, 2018
Na Msemaji Mkuu

Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari MAELEZO Bi.  Zamaradi  Kawawa akifungua mafunzo ya uandishi wa habari za takwimu kwa waandishi wa habari wa Jiji  la   Dodoma leo  kwa niaba ya Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi.

Mkurugenzi  Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt.  Albina    Chuwa akisisitiza kuhusu  namna idadi ya watu inavyoongezeka au kupungua wakati  wa  mafunzo ya uandishi wa habari za takwimu kwa waandishi wa habari wa Jiji la  Dodoma leo.

Mtakwimu kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Bw. Omary Mdoka akiwasilisha mada kuhusu ongezeko la watu  wakati   wa  mafunzo ya uandishi wa habari za takwimu kwa waandishi wa habari wa Jiji la  Dodoma leo.

Mwanasheria wa Ofisi ya  Taifa ya Takwimu (NBS) Bw. Oscar Mangula akiwasilisha mada kuhusu Sheria ya takwimu ya mwaka 2015 wakati  wa  mafunzo ya uandishi wa habari za takwimu kwa waandishi wa habari wa Jiji la  Dodoma leo.

Mmoja wa washiriki wa mafunzo ya uandishi wa habari za kitakwimu Bw. Magnus Mahenge akizungumza wakati wa mafunzo hayo leo Jijini Dodoma.

Mtakwimu  kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu Bi.  Mariam Kitembe akisisitiza jambo wakati akiwasilisha mada kuhusu hali ya maambukizi ya Virusi vya Ukimwi hapa nchini kwa kuzingatia utafiti uliofanyika mwaka 2016/2017 wakati  wa  mafunzo ya uandishi wa habari za takwimu kwa waandishi wa habari wa Jiji la  Dodoma leo.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu  (NBS) Bw. Said Ameir akitoa maelezo kuhusu  mafunzo ya siku mbili  ya uandishi wa habari za takwimu kwa waandishi wa habari wa Jiji la  Dodoma leo wakati wa mafunzo hayo ya siku mbili.

Mkurugenzi wa shughuli za kitakwimu kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu  Bw. Irenius Ruyobya akisisitiza jambo   wakati  wa  mafunzo ya uandishi wa habari za takwimu kwa waandishi wa habari wa Jiji la  Dodoma leo.

Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari MAELEZO Bi.  Zamaradi  Kawawa ambaye alikuwa mgeni rasmi  kwa niaba  ya Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo ya uandishi wa habari za takwimu kwa waandishi wa habari wa Jiji la  Dodoma leo.

(Picha zote na Frank Mvungi)

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi