Elisa Rwamiago, Afisa Msimamizi wa Fedha Mwandamizi TAMISEMI akitoa maelezo kabla ya kufunguliwa kwa mafunzo ya Mfumo wa Usimamizi wa Fedha za Umma (EPICPOR) Toleo la 10.2.
Mwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza, Isabella Marick, Katibu Tawala Msaidizi Sekta ya Mipango na Uratibu akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Mfumo wa Usimamizi wa Fedha za Umma kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa.
Meneja Mradi wa PS3 Mkoa wa Mwanza, Palestian Masai akitoa neno la ukaribisho kwa washiriki wa mafunzo ya Mfumo wa Usimamizi wa Fedha za Umma.
Wahasibu na Maafisa Usimamizi wa Fedha kutoka Halmashauri za Mwanza na Simiyu wakijitambulisha wakati wa mafunzo ya Mfumo wa Fedha za Umma (EPICPOR) Toleo la 10.2
Washiriki wa Mafunzo wakifuatilia kwa makini wakati wa mafunzo ya Mfumo wa fedha za umma kwa siku ya kwanza Mkoani Mwanza.
Timu ya wakufunzi wakifuatilia uwasilishaji wa mada wakati wa mafunzo kutoka kwa Mkufunzi mkuu wa Mafunzo ya Mfumo wa Usimamizi wa Fedha za Umma (EPICPOR) Toleo la 10.2