Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Matukio Katika Picha Hafla ya Kufunga Mafunzo ya Mfumo wa Epicor 10.2 kwa Maafisa Ugavi Jijini Mbeya
Jun 09, 2018
Na Msemaji Mkuu

Sehemu ya washiriki wa mafunzo ya matumizi ya mfumo wa Epicor 10.2 yanayowashirikisha  Maafisa Ugavi wa mikoa ya Mbeya, Njombe, Rukwa na Songwe kama wanavyoonekana wakifuatilia  hafla ya kufunga mafunzo hayo  leo  yaliyofanyika kwa siku mbili  Jijini Mbeya.

Afisa TEHAMA kutoka Ofisi ya  Rais,Tawala la Mikoa na Serikali za Mitaa  (TAMISEMI) Bw. Malowa Hamimu akizungumzia umuhimu wa maafisa ugavi kuzingatia mafunzo ya mfumo wa Epicor 10.2 wakati wa hafla ya kufunga mafunzo hayo Jijini Mbeya Leo ambapo yaliwashirikisha maafisa hao kutoka mikoa ya Songwe,  Mbeya, Njombe, Rukwa na  Katavi

Afisa ugavi kutoka halmashauri ya manispaa ya Sumbawanga Bw. Martin Sanane ambaye alikuwa mwenyekiti wa mafunzo ya matumizi ya mfumo wa Epicor 10.2 yanayowashirikisha  maafisa ugavi wa mikoa ya Mbeya, Njombe, Rukwa na Songwe akizungumzia wajibu wa maafisa hao katika kutumia mfumo huo wakati wa hafla ya kufunga mafunzo hayo yaliyofanyika kwa siku mbili  Jijini Mbeya. Afisa TEHAMA kutoka Ofisi ya  Rais,Tawala la Mikoa na Serikali za Mitaa  (TAMISEMI) Bw. Malowa Hamimu akisitiza umuhimu wa kuzingatia taratibu zinazotakiwa katika kutumia mfumo wa Epicor 10.2 kwa maafisa ugavi wa mikoa ya Mbeya, Njombe, Rukwa na Songwe akizungumzia wajibu wa maafisa hao katika kutumia mfumo huo kabla ya  hafla ya kufunga mafunzo hayo yaliyofanyika kwa siku mbili  Jijini Mbeya

Afisa Ugavi kutoka  Halmashauri ya Wilaya ya Kyela Bw. Godfrey  Sanga akieleza faida za mfumo wa Epicor 10.2 mara baada ya hafla ya kufunga mafunzo kwa maafisa ugavi wa mikoa ya Mbeya, Njombe, Rukwa na Songwe akizungumzia wajibu wa maafisa hao katika kutumia mfumo huo yaliyofanyika kwa siku mbili  Jijini Mbeya.

(Picha zote na Frank Mvungi MAELEZO, Mbeya )

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi