Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Matukio Katika Picha Bungeni Leo
Jun 01, 2018
Na Msemaji Mkuu

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof.   Palamagamba  Kabudi akizungumzia umuhimu wa kutunza  rasilimali za Taifa kwa maslahi ya kizazi hiki na kijacho wakati akichangia mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi   ya Wizara ya Madini kwa mwaka 2018/2019 leo Bungeni Mjini Dodoma.

Mbunge wa Muheza  Mhe. Balozi Adadi Rajabu akizungumzia mchango wa sekta ya madini wakati wa mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya Fedha ya Wizara ya Madini  leo Bungeni  Jijini Dodoma.

Mbunge wa  viti maalum Mkoa wa Singida Mhe.  Martha Mlata akizungumzia  umuhimu wa hatua zilizochukuliwa na Serikali katika kulinda rasilimali madini wakati wa mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Madini kwa mwaka 2018/ 2019.

Waziri wa Madini Mhe. Angellah Kairuki akitoa hotuba ya kufunga maonesho ya madini yaliyofanyika kwa siku mbili katika viwanja vya Bunge Jijini Dodoma.

Mjiolojia  Mwandamizi  kutoka   Wakala  wa  Jiolojia  na  Utafiti wa Madini (GST) Bw. Octavian Minja akisisitiza jambo  kwa mmoja wa wananchi waliotembelea maonesho ya Madini yaliyofanyika katika viwanja vya Bunge   Jijini Dodoma.

Sehemu ya washiriki wa maonesho ya madini yaliyofanyika katika viwanja vya Bunge wakisikiliza hotuba ya Waziri wa Madini wakati akifunga maonesho hayo leo Jijini Dodoma.

Mmoja  wa washiriki wa maonesho ya madini yaliyofanyika katika viwanja vya Bunge Jijini Dodoma Bi Susie Kennedy  akifurahia jambo na Waziri wa Madini  wakati akikabidhiwa cheti cha ushiriki wakati wa hafla yakufunga maonesho hayo leo Jijini Dodoma.

Sehemu ya wageni waliofika Bungeni wakifuatilia  kipindi cha maswali na  majibu Bungeni Jijini Dodoma leo.

Sehemu ya mabanda ya maonesho ya Madini kama inavyoonekana katika picha ndani ya Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma.

( Picha zote na Frank Mvungi- MAELEZO, Dodoma)

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi