Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Mashindano ya UMISSETA yafunguliwa rasmi Arusha.
May 23, 2017
Na Msemaji Mkuu

Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo (Mbele) akihutubia maelfu ya wanafunzi wa shule za Sekondari za jijini Arusha zinazoshiriki michuano ya Copa/UMISSETA, wakati wa ufunguzi wa mashindano hayo  yaliyofanyika  mwishoni mwa wiki kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid.  

Na Mwandishi Wetu

Kampuni ya vinywaji baridi ya Coca-Cola hapa nchini, kwa ushirikiano na TAMISEMI, imefanya uzinduzi wa mashindano ya umoja wa Shule za Sekondari (Umisseta) kwa kanda ya Kaskazini, mkoani Arusha kwa kugawa vifaa vya michezo kwa shule mbalimbali za Sekondari za Serikali na binafsi.

Katika uzinduzi wa mashindano hayo jijini Arusha, kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid mwishoni mwa wiki, mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo, ambapo aliishukuru kampuni ya Coca cola kwa udhamini kufanikisha michuano yam waka huu.

Kwa upande wake, Meneja Mauzo wa Coca-Cola Mkoa wa Arusha, Boniface Mwasi alisema kuwa kampuni hiyo imeona umuhimu wa kuibua vipaji vya michezo ndio maana wamejikita kufadhili michezo kama hiyo kwa vijana ikiwa ni katika kuisaidia Serikali katika azma yake ya kukuza michezo.

Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo (Kushoto) akisalimia moja ya timu ya shule za sekondari kutoka mkoa wa Arusha, katika ufunguzi wa mashindano ya Copa Umisseta mkoani hapa yaliyofanyika mwisho wa wiki katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid, ambapo kampuni ya vinywaji baridi ya Coca-Cola iligawa vifaa mbali mbali vya michezo kwa shule za Serikali na binafsi kwa ajili ya ushiriki wa michuano ya mwaka huu.
[caption id="" align="alignnone" width="640"] Baadhi ya wanafunzi wakiangalia mashindano ya mpira wa miguu wanafunzi wa shule za Sekondari za jijini Arusha zinazoshiriki michuano ya Copa/UMISSETA, wakati wa ufunguzi wa mashindano hayo yaliyofanyika mwishoni mwa wiki kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid.[/caption] “Tumeamua kushirikiana na Serikali katika michezo hii ya Umisseta lengo letu kubwa likiwa ni kuibua vipaji vingi vya michezo kwa kuwa tunaamini mtandao wa shule za Sekondari ni mkubwa na ni rahisi kuibua vipaji vingi kutoka sehemu zote za nchi”, Alisema Mwasi. Aidha, aliongeza kuwa kampuni ya Coca-Cola itaendelea kuunga mkono jitihaa za Serikali za kukuza sekta ya michezo nchini hususani katika ngazi za chini ambako imekuwa ni vigumu kupata ufadhili kwa kuwa tunaamini kuwa vipaji vinapaswa kuibuliwa na kukuzwa. “Tunayo dhamira ya kuona vijana wa kitanzania walioibukia kwenye mashindano haya wanafika mbali kimichezo na hatimaye kujipatia ajira na pia kuitangaza nchi kitaifa na kimataifa”, Alisisitiza Mwasi.    
    \   >

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi