Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Majaliwa Afungua Mkutano Mkuu wa 34 wa ALAT Jijini Dodoma
Sep 27, 2018
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_35814" align="aligncenter" width="750"] Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkurugenzi wa jiji la Dodoma, Godwin Kunambi wakati alipowasili kwenye ukumbi wa Jakaya Mrisho Kikwete kufungua Mkutano wa 34, wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa, Septemba 27, 2018. Kulia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mkoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo na kushoto ni Naibu Waziri wa Kilimo, Dkt, Mary Mwanjelwa. Watatu kushoto ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Josephat Kandege na watatu kulia ni Meya wa jiji la Dodoma, Profesa Davis Mwamfupe.[/caption] [caption id="attachment_35815" align="aligncenter" width="750"] Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kuhusu mitambo ya umeme kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Tekinolojia na Masoko wa REA, Elineema Mkumbo (wa pili kushoto) wakati alipotembelea banda la maonyesho la REA kabla ya kufungua Mkutano Mkuu wa 34 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Kwenye ukumbi wa Jakaya Mrisho Kikwete jijini Dodoma, Septemba 27, 2018.[/caption] [caption id="attachment_35817" align="aligncenter" width="750"] Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifungua Mkutano Mkuu wa 34 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa (ALAT) kwenye ukumbi wa Jakaya Mrisho Kikwete jijini Dodoma Septemba 27, 2018.[/caption] [caption id="attachment_35820" align="aligncenter" width="750"] Baadhi ya washiriki wa Mkutano Mkuu wa 34 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa (ALAT) wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipofungua Mkutano huo kwenye ukumbi wa Jakaya Mrisho Kikwete jijini Dodoma, Septemba 27, 2018.[/caption] [caption id="attachment_35822" align="aligncenter" width="750"] Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiagana na baadhi ya viongozi walioshiriki katika Mkutano Mkuu wa 34 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa (ALAT) Kwenye ukumbi wa Jakaya Mrisho Kikwete jijini Dodoma Septemba 27, 2018. Kulia ni Mwenyekiti wa ALAT, Gulaam Hafeez 'Mukadam', wapili kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Bilinith Mahenge na wanne kulia ni Naibu Waziri wa Kilimo, Dkt. Mary Mwanjelwa.[/caption]

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi