Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Maandalizi ya Mkutano wa Mawaziri na Wadau wa Utatu wa Sekta ya Kazi na Ajira wa SADC yakamilika
Mar 01, 2020
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_51298" align="aligncenter" width="750"] Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana, na Wenyeulemavu, Jenista Mhagama akiangalia ramani ya Safari za Wafanyabiashara ya watumwa iliyoko katika jumba la makumbusho(Caravan Serai) lililoko Bagamoyo ambalo lilitumiwa na wafanyabiashara hao kama sehemu ya kupumzika baada ya kusafirisha watumwa kwa umbali mrefu kutoka nchi za Kusini mwa Afrika, baada ya kutembelea maeneo hayo kwa ajili ya kukagua maeneo watakayotembelea mawaziri wa Mkutano wa Mawaziri na Wadau wa Utatu wa Sekta ya Kazi na Ajira wa SADC.[/caption] [caption id="attachment_51299" align="aligncenter" width="750"] Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira Vijana, na Wenyeulemavu, Jenista Mhagama, akipokea maelezo kutoka kwa mwongoza watalii wa jumba la makumbusho(Caravan Serai) lililoko Bagamoyo kwa ajili ya kukagua maeneo watakayotembelea mawaziri wa Mkutano wa Mawaziri na Wadau wa Utatu wa Sekta ya Kazi na Ajira wa SADC.[/caption] [caption id="attachment_51300" align="aligncenter" width="750"] Moja ya picha ikionesha mtumwa amebeba pembe za ndovu katika kituo walichokuwa wakipumzika katika moja jumba la makumbusho(Caravan Serai) lililoko Bagamaoyo ambalo lilitumiwa na wafanyabiashara hao kama sehemu ya kupumzika baada ya kusafirisha watumwa kwa umbali mrefu kutoka nchi za Kusini mwa Afrika.[/caption] [caption id="attachment_51301" align="aligncenter" width="750"] Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi,Ajira Vijana, na Wenyeulemavu, Jenista Mhagama akimsikiliza mwongoza watalii alipokuwa akieleza kuhusu jumba la Ngome Kongwe lililoko Bagamoyo ambalo lilitumiwa na wafanyabiashara ya utumwa kama sehemu ya kupumzika kabla ya kupeleka watumwa katika soko dogo la watumwa lililokuwa Bagamoyo, katika mwendelezo wa kukagua maeneo watakayotembelea mawaziri wa Mkutano wa Mawaziri na Wadau wa Utatu wa Sekta ya Kazi na Ajira wa SADC.[/caption] [caption id="attachment_51302" align="aligncenter" width="750"] Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana, na Walemavu, Jenista Mhagama akimsikiliza mwongoza watalii alipokuwa akieleza kuhusu bandari iliyotumika kusafirisha watumwa kwenda Zanzibar iliyoko Bagamoyo ambalo bandari hiyo ilitumiwa sana na wafanyabiashara ya utumwa kama Sehemu kupeleka watumwa katika soko Kuu la Watumwa lilokuwa Zanzibar, baada ya kutembelea maeneo hayo ikiwa ni moja ya maandalizi ya Mkutano wa Mawaziri na Wadau wa Utatu wa Sekta ya Kazi na Ajira wa SADC.[/caption] [caption id="attachment_51303" align="aligncenter" width="750"] Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana, na Wenyeulemavu, Jenista Mhagama akimsikiliza mwongoza watalii alipokuwa akieleza kuhusu jumba la makumbusho ya Kanisa Katoliki lililoko Bagamoyo ambalo linaelezea juhudi za kukomesha biashara ya utumwa.[/caption] [caption id="attachment_51304" align="aligncenter" width="750"] Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi,Ajira, Vijana, na Wenyeulemavu, Jenista Mhagama, akisoma moja ya kumbukumbu iliyoko kwenye jumba la makumbusho ya Kanisa Katoliki lililoko Bagamoyo[/caption] [caption id="attachment_51305" align="aligncenter" width="750"] Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana, na Wenyeulemavu, Jenista Mhagama akiwa na baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Mkutano wa Mawaziri na Wadau wa Utatu wa Sekta ya Kazi na Ajira wa SADC, akisikiliza maelezo kuhusu nyumba aliyokuwa akiishi mpigania uhuru wa Msumbiji, Hayati Samora Machael iliyoko Bagamoyo mkoani Pwani walipotembelea leo kukamilisha maandalizi ya Mkutano huo utakaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, Tanzania[/caption] [caption id="attachment_51306" align="aligncenter" width="750"] Nyumba alimokuwa akiishi mpigania uhuru wa Msumbiji, Hayati Samora Machael iliyoko Bagamoyo Mkoani Pwani, mara baada ya kutembelewa leo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana, na Walemavu, Jenista Mhagama akiwa na Wajumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Mkutano wa Mawaziri na Wadau wa Utatu wa Sekta ya Kazi na Ajira wa SADC utakaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, Tanzania.[/caption] [caption id="attachment_51307" align="aligncenter" width="750"] Moja ya eneo kongwe la makumbusho la Kaole lililoko Bagamoyo Mkoani Pwani kama linavyoonekana kwenye picha mara baada ya kutembelewa leo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana, na Wenyeulemavu, Jenista Mhagama akiwa na Wajumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Mkutano wa Mawaziri na Wadau wa Utatu wa Sekta ya Kazi na Ajira wa SADC utakaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, Tanzania.[/caption] [caption id="attachment_51308" align="aligncenter" width="750"] Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana, na Wenyeulemavu, Jenista Mhagama akiwa na Wajumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Mkutano wa Mawaziri na Wadau wa Utatu wa Sekta ya Kazi na Ajira wa SADC wakimsikiliza mwongoza watalii wa makumbusho ya Kaole, Mkutano huo utafanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, Tanzania.[/caption] [caption id="attachment_51309" align="aligncenter" width="750"] Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira Vijana, na Wenyeulemavu, Jenista Mhagama akiwa na Wajumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Mkutano wa Mawaziri na Wadau wa Utatu wa Sekta ya Kazi na Ajira wa SADC wakiangalia maji ya kisima kilichopo katika makumbusho ya Kaole, Mkutano huo utafanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, Tanzania.[/caption] [caption id="attachment_51310" align="aligncenter" width="750"] Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana, na Walemavu, Jenista Mhagama akionesha kaburi la wapendanao kwa Wajumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Mkutano wa Mawaziri na Wadau wa Utatu wa Sekta ya Kazi na Ajira wa SADC katika makumbusho ya mambo ya kale Kaole, Mkutano huo utafanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, Tanzania.[/caption] [caption id="attachment_51312" align="aligncenter" width="750"] Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi,Ajira Vijana, na Wenyeulemavu, Jenista Mhagama akiwa na Wajumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Mkutano wa Mawaziri na Wadau wa Utatu wa Sekta ya Kazi na Ajira wa SADC wakipata maelezo kuhusu makaburi ya watoto wadogo waliofariki yaliyoko katika makumbusho ya mambo ya kale Kaole Bagamoyo Pwani, Mkutano huo utafanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, Tanzania.[/caption]

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi