Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Yakagua Ujenzi wa Kiwanda cha Mataruma cha SGR
Mar 14, 2022
Na
Jacquiline Mrisho
Meneja Mradi wa Mradi wa Reli ya Kisasa ya SGR, sehemu ya Mwanza-Isaka (KM 341), Mhandisi Masanja Machibya akifafanua kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Selemani Kakoso (Kulia) na wajumbe wa kamati kuhusu hatua mbalimbali za ujenzi wa Kiwanda cha mataruma cha reli ya Kisasa ya SGR, kinachojengwa wilayani Kishapu, mkoani Shinyanga wakati kamati hiyo ilipotembelea mradi huo mwishoni mwa wiki.
Muonekano wa kipande cha Reli ya Kisasa ya SGR, sehemu ya Mwanza-Isaka (KM 341) kilichotandikwa katika eneo la Seke, wilayani Kishapu, mkoani Shinyanga.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Selemani Kakoso akitoa maelekezo kwa Uongozi wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), wakati Kamati hiyo ilipotembelea Mradi wa Reli ya Kisasa ya SGR, sehemu ya Mwanza-Isaka (KM 341) eneo la Seke, wilayani Kishapu, mkoani Shinyanga.
Muonekano wa hatua za awali za ujenzi wa Kiwanda cha mataruma cha reli ya Kisasa ya SGR, kinachojengwa wilayani Kishapu, mkoani Shinyanga. Kiwanda hicho ni sehemu ya mradi wa Mwanza-Isaka (KM 341) ambapo ujenzi wake umefikia asilimia 4.