Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Viongozi wa Taasisi Washauriwa Kupima Afya Kila Mara
Jun 09, 2017
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_3119" align="aligncenter" width="750"] Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akiwaelezea wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) umuhimu wa kupima afya zao mara kwa mara japo mara moja kwa mwaka wakati wafanyakazi hao walipofika katika Taasisi hiyo leo kwa ajili ya upimaji wa afya zao.[/caption]

Na Anna Nkinda - JKCI

Viongozi wa mashirika ya Umma na Binafsi wametakiwa kujenga mazoea ya kupima afya zao mara kwa mara ili waweze kujua hali ya afya zao na ikijulikana kama wana magonjwa basi waweze kupatiwa matibabu kwa wakati.

Rai hiyo imetolewa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi wakati akiongea na viongozi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) waliofika katika Taasisi hiyo kwa ajili ya upimaji wa Afya zao.

Prof. Janabi alisema baadhi ya viongozi  hawana mazoea ya kupima afya zao japo mara moja kwa mwaka na inapotokea wamegundulika  kuwa na tatizo  la ugonjwa huwa ni  kubwa na limeshaleta madhara mwilini   na wakati  mwingine huwa  ni vigumu kutibika.

[caption id="attachment_3120" align="aligncenter" width="750"] Mkurugenzi wa Ukaguzi wa Hesabu kutoka Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Fatuma Chillo akiuliza ni muda gani mzuri wa kupima shinikizo la damu mwilini (BP) wakati wafanyakazi wa shirika hilo walipofika katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya upimaji wa afya zao. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Sheria na Katibu wa NHC Martin Mdoe.[/caption]

Akizungumzia kuhusu magonjwa ya Moyo, Mkurugenzi Mtendaji huyo alisema ni muhimu mgonjwa afuate maelekezo ya jinsi ya kutumia dawa aliyopewa na daktari wake kwani kuna baadhi ya wagonjwa wamekuwa na tabia ya kuacha kutumia dawa pindi wanapojiona wamepata naafuu jambo ambalo siyo sahihi.

Akielezea jinsi ya kujikinga na magonjwa ya Moyo kwa upande wa chakula Afisa Lishe kutoka JKCI, Louisa Shem alisema ni muhimu kupunguza utumiaji wa vyakula vya mafuta kupita kiasi hasa mafuta yatokananyo na wanyama, kutumia vyakula vya nafaka zisizokobolewa.

Kupunguza unywaji wa pombe na uvutaji wa bidhaa zitokanazo na tumbaku ikiwemo sigara, kufanya mazoezi ya mwili angalau nusu saa kwa siku na kupunguza matumizi ya vyakula vyenye chumvi nyingi.

[caption id="attachment_3121" align="aligncenter" width="750"] Mkurugenzi wa Ukaguzi wa Hesabu kutoka Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Fatuma Chillo akichukuliwa kipimo cha damu na Alex Onesmo kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa magonjwa mbalimbali ikiwemo Moyo, figo na kisukari. Viongozi wa NHC walifika katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) leo kwa ajili ya upimaji wa afya zao.[/caption] [caption id="attachment_3122" align="aligncenter" width="584"] Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Edna Kajuna akimpima urefu na uzito Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Mkoa wa Mwanza Benedict Kilimba wakati viongozi wa Taasisi hiyo walipofika katika Taasisi hiyo leo kwa ajili ya upimaji wa afya zao.[/caption] [caption id="attachment_3123" align="aligncenter" width="750"] Mkurugenzi wa Ubunifu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Peter Issack akichukuliwa kipimo cha damu na Alex Onesmo kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa magonjwa mbalimbali ikiwemo Moyo, figo, tezi dume na kisukari. Viongozi wa NHC walifika katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) leo kwa ajili ya upimaji wa afya zao.[/caption]

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Afya na Usalama Kazini kutoka  NHC Dkt. Yothan Mackenzie  alisema hivi karibuni walikuwa na mkutano wa Baraza la Wafanyakazi katika mkutano huo kulikuwa na mada ya ulaji na afya wakaona ni vyema mada hiyo iende sambamba na upimaji wa magonjwa mbalimbali ikiwemo ugonjwa wa Moyo.

Dr. Mackenzie alisema wanawapima viongozi hao kwa awamu hadi sasa jumla ya wakurugenzi na wakuu wa vitengo 14 wamepima na kujuwa afya zao na viongozi wengine wataendelea kupima kwani wanaamini kuwa mfanyakazi akiwa na afya njema ataweza kufanya kazi zake vizuri.

Baadhi ya magonjwa waliyopima viongozi hao ni pamoja na Moyo, tezi dume, figo na sukari.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi