Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Fedha Tozo za Miamala za Siku 45 Kujenga Vituo vya Afya 220
Sep 01, 2021
Na Jacquiline Mrisho

Na Redempta Ndubuja

Serikali imejipanga kujenga Vituo vya Afya 220 kwenye Tarafa ambazo hazijawahi kuwa na  vituo hivyo tangu kupata Uhuru .

 Hayo  yamesemwa  leo`Jijini  Dodoma  na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Mwigulu  Nchemba  alipokuwa anazungumza  na Waandishi wa Habari kuhusu viwango vya tozo vilivyopunguzwa kwenye miamala.

“Wakati Rais Samia anapokea kijiti kulikuwa na Tarafa 217 ambazo hazikuwa na Vituo vya Afya hivyo tumeweka malengo ya kufikia vituo 220, kwa maana hiyo ndani ya siku 45 ambazo tumekusanya fedha kutoka katika miamala ya simu tumepata fedha za kujengea vituo 220 kwenye Tarafa ambazo hazikuwa na vituo hivyo”, alisema Dkt. Mwigulu

Kuna watu wanapenda kujiita masikini lakini hawa waliopo Vijijini ambao wanaweza kupoteza maisha kwa sababu hakuna  hospitali karibu nao ndio  Rais Samia anakwenda kuwagusa, wale waliopo Mijini wanaweza kuchagua waende hospitali ipi iwe za Serikali au Binafsi,” alisisitiza Mwigulu.

Aidha, amesema vituo 220 vitakavyojengwa katika Tarafa zote vitakuwa na wodi za wanawake na watoto pia vitakuwa na uwezo wa kufanya upasuaji utakaopelekea kuokoa maisha ya wananchi wengi.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi