Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

CAG Yakoa Shilingi Bilioni 1.45
Mar 26, 2020
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_51832" align="aligncenter" width="750"] Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipima joto la mwili kabla ya kuingia katika ukumbi wa Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma kwa ajili ya kupokea Taarifa ya CAG kwa Mwaka 2018/2019 pamoja na Taarifa ya TAKUKURU leo tarehe 26/03/2020.[/caption]

Na Jonas Kamaleki, Dodoma

Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) imeokoa jumla ya Shilingi bilioni 1.45 ambayo ingelipwa kama ada ya ukaguzi kwa makampuni binafsi ya ukaguzi.

Hayo yamebainishwa leo Ikulu ya Chamwino, Dodoma na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali, Charles Kichere wakati akiwasilisha Ripoti ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali ya mwaka 2018/19 kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.

[caption id="attachment_51833" align="aligncenter" width="750"] Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akipima joto la mwili kabla ya kuingia katika ukumbi wa Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.[/caption]

Kichere amesema ofisi yake imeokoa fedha hizo kwa kutumia wakaguzi wa ofisi yake kukagua mashirika ya umma ambayo baadhi yake ni TANAPA, BOT, SUA, TTCL na TIC.

“ Mheshimiwa Rais ofsi yangu imejipanga kukagua mashirika mengine makubwa kama vile Mamlaka ya Hifadhi Ngorongoro, EWURA, Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu, Tanesco, Chuo Kikuu cha Ardhi, Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Shirika la Ndege la Taifa (ATCL) na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC),” amesema Kichere.

[caption id="attachment_51834" align="aligncenter" width="750"] Spika wa Bunge Job Ndugai akipima joto la mwili kabla ya kuingia katika ukumbi wa Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.[/caption]

Kutokana na uhaba wa watumishi katika ofisi ya CAG, Rais Magufuli ameiagiza Utumishi kutoa kibali cha ajira ya watumishi 25 katika ofisi hiyo.

“CAG nakupongeza sana kwa kuanza kukagua mashirika yetu ya umma kwa kutumia watu wetu, ni kitendo cha kizalendo, umefanya vizuri,” amesema Rais Magufuli

Aidha, Rais Magufuli amemthibitisha aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kumpambana na Rushwa (TAKUKURU), Brigedia Jenerali, John Mbungo kuwa Mkurugenzi MKuu wa TAKUKURU kutokana na kazi aliyoifanya ya kurudisha bilioni 8.8 za wananchi.

[caption id="attachment_51836" align="aligncenter" width="750"] Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan mara baada ya kutoka kwenye ukumbi wa Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma ambapo alipokea Ripoti mbili za Mwaka 2018/2019 kutoka Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa PCCB pamoja na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali CAG.[/caption]

Rais Magufuli amemuhakikishia Mhe. Spika, Job Ndugai kuwa Ripoti ya CAG itawasilishwa bungeni jinsi ilivyo bila kubadilishwa kwa namna yoyote ili ijadiliwe na wabunge kwa mujibu wa sheria.

CAG na TAKUKURU wamewasilisha Ripoti zao leo kwa Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Ikulu ya Chamwino Dodoma.

[caption id="attachment_51837" align="aligncenter" width="750"] Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, Spika wa Bunge Job Ndugai wakwanza kushoto waliokaa, akifatiwa na CAG Charles Kichere, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Brigedia Jenerali John Mbungo wapili kutoka kulia waliokaa pamoja na Wafanyakazi wa Ofisi ya TAKUKURU na CAG, Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.[/caption] [caption id="attachment_51831" align="aligncenter" width="750"] . Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali CAG Charles Kichere akisoma Muhtasari wa Taarifa yake ya Mwaka 2018/2019 katika Ikulu ya Chamwino mkoani[/caption]

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi