Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Biashara Tanzania, India Yakua kwa Dola za Marekani Bilioni 3.1.
Oct 09, 2023
Biashara Tanzania, India Yakua kwa Dola za Marekani Bilioni 3.1.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan pamoja na ujumbe wake akiwa na Waziri Mkuu wa India, Mhe. Narendra Modi katika mazungumzo rasmi katika Jengo Maalum la kupokelea wageni wa Kitaifa Hyderabad House New Delhi Nchini India tarehe 09 Oktoba, 2023.
Na Paschal Dotto-MAELEZO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema Biashara kati ya Tanzania na India imekua na kufikia dola za kimarekani bilioni 3.1 kwa mwaka 2022.

Akizungumza katika ziara ya Kikazi aliyoifanya nchini India Oktoba 9, 2023 Rais Samia amesema kuwa Tanzania na India zina ushirikiano wa kihistoria wa miaka mingi na kwamba ushirikiano huo umefanya biashara kati ya nchi hizo mbili kukua.

"Napenda kutoa shukrani kwa Serikali na Watu wa India kwa ushirikiano wenu wa miaka mingi  katika sekta mbalimbali, kwenye sekta ya biashara kati ya Tanzania na India imekua na kufikia dola za kimarekani bilioni 3.1 mwaka 2022 na kufanya India kuwa namba 3 kwenye eneo hilo lakini pia kuwa namba 5 kati ya nchi zilizowekeza nchini kwetu,” amesema Mhe. Rais Samia.

Ameendelea kusema kuwa Tanzania itaendelea kufungua fursa zaidi za ushirikiano na India kwenye maendeleo ya kiuchumi na kisiasa huku akiipongeza India kuwa Mwenyeji wa Mkutano wa G-20.

Aidha, Rais Samia alimshukuru Waziri Mkuu wa India, Mhe. Narendra Modi kwa ukarimu na ukaribisho mzuri waliouonesha kwake pamoja na ugeni wake nchini humo

Aliongeza kuwa Tanzania na India zinaendelea kufurahia ushirikiano wa miaka mingi ambao ni wa kihistoria na ziara hiyo inathibitisha utayari wa Tanzania kuendelea kuimarisha urafiki huo.
 

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi